Thursday, July 25, 2013

STARS YAWASILI UGANDA TAYARI KUIKABILI CRANES


Baadhi ya wachezaji wa timu ya taifa, Taifa Stars na benchi la ufundi wakiwasili katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Entebe nchini Uganda jana tayari kwa mchezo wa marudiano na timu ya Taifa ya Uganda Jumamosi hii.
Timu ya Taifa (Taifa Stars) imewasili Uganda jioni hii Jumatano tayari kuikabili Uganda Cranes kwa mechi ya marudiano kutafuta tiketi ya kucheza katika mashindano ya CHAN.
 
Kikosi hicho chichi nye wachezaji 20, kiliwasili muda mfupi baada ya saa kumi alasiri huku wachezaji na benchi la ufundi wakiwa na matumaini makubwa.
 
Akiongea mara baada ya kuwasili Kocha wa Timu ya Taifa Kim Poulsen alisema wamejiandaa vizuri wakiwa Mwanza na ana imanikikosi hiki kitabadili atokeo ya awali ambapo Stars ilifungwa 1-0 na Cranes Jijini Dar es Salaam.
 
Alisema licha ya kuwakosa wachezaji Shomari kapombe na Mwinyi Kazimoto, ana imani na kikosi chake hiki kuwa kitafanya makubwa Kampala.
 
“Tumekuja kubadilisha mahesabu kwani tumejiandaa vizuri kabisa,” alisema Poulsen.
 
Wadhamini wa Stars, Kilimanjaro Premium Lager wamewaomba watanzania wasikate tama kwani Stars bado ina nafasi kubwa ya kupindua meza.
 
“Sisi kama wadhamini bado tuna imani na Stars na tunajua watatuwakilisha vizuri ni vyema watanzania wawe na imani na kuiombea dua timu iibuke na ushindi mnono katika mechi hii ya marudiano,” alisema Meneja wa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, george Kavishe.
 
Mechi hii ni gumzo kubwa Jijini Kampala kwani baadhi ya waganda wana hofu kuwa henda wakafungwa nyumbani kwao.
 
Mechi hii itapigwa katika Uwanja wa Nambole Jijini Kampala JUmamosi hii saa kumi jioni.
 
Mashindano ya CHAN yanatarajiwa kufanyika Januari mwakani nchini Afrika Kusini.
 
 

No comments: