Wednesday, July 10, 2013

NHC YAMPIGA TAFU MISS TANZANIA 2012 KUJENGA BWENI LA ALBINO BUHANGIJA

Miss Tanzania 2012, Brigitte Alfred (kulia) akipokea hundi yenye thamani ya shilingi Milioni 4.1 kutoka kwa Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Huduma kwa Jamii wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Susan Omari jijini Dar es Salaam jana. Fedha hizo ni kwaajili ya ujenzi wa Bweni la wanafunzi wenye ulemavu wa ngozi (Albino) linalojengwa katika shule ya Msingi Buhangija mkoani Shinyanga. Fedha hizo ni maalum kwaajili ya kununulia mabati ya kuezekea bweni hilo. Kwa mujibu wa Brigitte zaidi ya Shilingi milioni 60 zinahitajika kukamilisha ujenzi huo.

No comments:

WIZARA YA AFYA YAOMBA SH. TRILIONI 1.8 BAJETI YA 2026/2027

  Wizara ya Afya imeomba kuidhinishiwa jumla ya Shilingi trilioni 1.8 kwa mwaka wa fedha 2026/2027 kwa ajili ya kuendelea kuboresha huduma z...