Monday, July 29, 2013

UWAKILISHI WA KUDUMU WA NEW YORK WAMUAGA BALOZI MERO


Moja ya Zawadi ambazo wafanyakazi wa Ubalozi wa Tanzania Umoja wa Mataifa waliyomizawadia Bw. Mero kama kumbukumbu, kutoka kushoto ni Balozi Tuvako Manongi na mkewe Upendo, Balozi Modest Mero na mkewe Rose.
***********************************
Uwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, mwishoni mwa wiki uliandaa hafla fupi ya kumuaga Afisa mwenza Bw. Modest Mero na Familia yake, Bw. Mero aliteuliwa hivi karibuni na Mhe. Rais Jakaya Kikwete kuwa Balozi wa Tanzania Geneva, hafla hiyo ilifanyika katika Makazi ya Balozi Tuvako Manongi yaliyoko 86 Jadison. zifuatato ni baadhi tu ya picha ya hafla hiyo iliyoambatana na nyama choma na chakula cha jioni.
Muwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Tuvako Manongi, akizungumza machache wakati wa hafla hiyo ambapo alimuelezea Balozi Mero kama mchapa kazi , anayejituma na wakati wowote alipohitaji au kuulizwa chochote alilkuwa tayari kukifanya au kujibu.
Balozi Modest Jonadhan Mero akiwa na Mke wake, Bibi Rose Mero.

No comments: