Monday, July 29, 2013

NHC yasaidia Hospitali ya Usangi

 Meneja Huduma kwa Jamii wa NHC , Muungano Kasibi Saguya (katikati) pamoja na Meneja wa NHC mkoa wa Kilimanjaro, Sheikh Kombo (kulia)wakimsalimia mmoja wa wagonjwa waliolazwa katika jengo la upasuaji la Hospitali ya Wilaya ya Mwanga mkoani Kilimanjaro.
Jengo la upasuaji la Hospitali ya wilaya ya Usangi mkoani Kilimanjaro, lililofanyiwa ukarabati na NHC hivi karibuni.
Sehemu ya Hospitali ya wilaya ya Usangi mkoani Kilimanjaro, ambapo jengo lake moja limefanyiwa ukarabati na NHC hivi karibuni.
Meneja Huduma kwa Jamii wa NHC , Muungano Kasibi Saguya (wa kwanza mbele) wakishuhudia wagonjwa katika vitanda vilivyonakshiwa na shuka za Shirika la Nyumba la Taifa, wagonjwa hao wamelazwa  katika jengo la upasuaji la Hospitali ya Wilaya ya Mwanga mkoani Kilimanjaro, .
Meneja Huduma kwa Jamii wa NHC , Muungano Kasibi Saguya (kulia) akiwa ameshikilia mojawapo ya shuka zilizotolewa na Shirika la Nyumba la Taifa. Jumla ya shuka 160 zilitolewa na Shirika hilo.Kushoto ni Mganga Mkuu wa Wilaya ya Mwanga, Dk Gina Kagina
Meneja Huduma kwa Jamii wa NHC , Muungano Kasibi Saguya (kulia) akifungua pazia kuashiria uzinduzi wa jengo la upasuaji lililokarabatiwa na NHC hivi karibuni.
 Wafanyakazi wa NHC wakipata maelezo kutoka kwa Mganga Mkuu wa Wilaya ya Mwanga, Dk Gina Kagina.

Na Joyce Anael, Mwanga
SHIRIKA la Nyumba la Taifa (NHC) mkoani Kilimanjaro, limetumia zaidi ya Sh 16 milioni kukarabati jengo la upasuaji na na kununua mashuka kwaajili ya Hospitali ya wilaya ya Usangi mkoani Kilimanjaro, lengo likiwa ni kusaidia jamii kupata huduma bora za afya.
Akikabidhi jingo hilo juzi kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Meneja Huduma kwa Jamii, Muungano Saguya, alisema ukarabati huo ni moja ya mikakati ya SHirika katika kuhakikisha kila Mtanzania ananufaika na rasilimali za taifa.
Alisema shirika hilo limekuwa likitoa huduma mbalimbali kwa jamii ikiwemo katika sekta ya afya na elimu, ambapo misaada iyo inatokana na mapato ya kodi yanayolipwa na wapangaji wa nyumza za Shirika hilo katika maeneo mbalimbali nchini.
“Namna pekee ya kuwawezesha Watanzania wasio wapangaji wa nyumba za NHC ni kupitia msaada kama huu wa leo, Niwapongeze wapangaji wa nyumba za shirika mkoani Kilimanjaro kwa kubadili mwenendo wao na kuwa walipaji wazuri wa kodi nah ii iwe kielelezo tosha kuwa Shirika hili letu likiungwa mkono linafanya mambo mengi yenye manufaa kwa wananchi,”alisema Saguya.
Aidha, Meneja huyo aliutaka uongozi wa Hospitali ya Usangi, ambayo ndiyo Hospitali ya Wilaya ya Mwanga kulitunza jengo hilo ili liweze kudumu kwa muda refu kulingana na thamani iliyotumika katika ukarabati.
Alisema kutokana na uchakavu uliokuwepo, jengo hilo lilikosa sifa ya kufanyika kwa huduma ya upasuaji, lakini sasa hospitali hiyo inaweza kujivunia kufanya huduma hiyo baada ya ukarabati huo.
Meneja wa NHC mkoa wa Kilimanjaro, Shehe Kombo, alisema mradi wa ukarabati jingo hilo hususan upauaji ulianza Julai Mosi mwaka huu, ukarabati ambao uligharimu Sh 14 milioni.
Alisema baada ya ukarabati wa jingo hilo, Shirika la Nyumba lilikaa na kutathmini changamoto zinzoikabili hospitali hiyo ya wilaya na kutoa msaada mwingine wa shuka 160 ambazo zimegharimu Sh 2,350,000.
Naye Mganga Mkuu wa Wilaya ya Mwanga, Dk Gina Kagina alilishukuru shirika hilo kwa kuona umuhimu wa kukarabati jingo hilo la upasuaji ambalo lilikuwa na hali mbaya kabla ya kufanyiwa ukarabati.
Pia alisema kuwa bado kumekuwapo na changamoto nyingi katika hospitali hiyo ya wilaya ikiwamo uchakavu wa majengo, hivyo kuliomba shirika hilo kuona umuhimu wa kurudi katika hospitali hiyo na kutoa msaada mwingine.

No comments: