Tuesday, July 16, 2013

Chadema Yashinda Kwa Kishindo Kata Zake Nne Kwenye Uchaguzi Mdogo wa Udiwani Arusha,Soma Matokeo Kamili Yalivyokua Hapa



Wafuasi wa Chadema Wakishangilia Ushindi
--
MATOKEO NI KAMA IFWATAVYO
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), `kimefunika' katika uchaguzi 
mdogo wa madiwani uliofanyika kwenye kata nne za Jimbo la Arusha Mjini uliofanyika 
Jumapili.
Matokeo katika vituo mbalimbali vya kata hizo nne ambayo kwa mujibu wa  
 Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec), yalionyesha Chadema ikiongoza kwa idadi kubwa ya 
kura zilizopigwa kwenye vituo 136 vya kupigia kura huku kikifuatiwa na Chama Cha 
Mapinduzi (CCM).


Matokeo kamili katika vituo hivyo yalikuwa kama ifuatavyo:-

KATA YA KALOLENI:
Matokeo ya jumla Chadema 1,470, CCM 530, CUF 275 na Demokrasia Makini 2, 
 Kwa matokeo hayo Emmanuel Kessy wa Chadema alitangazwa mshindi.
Kituo kidogo A, Chadema kilikuwa kimenyakua kura 51, CCM 25 na CUF 11.
Kituo B1, Chadema 68, CCM 19 na CUF 17 huku katika kituo A4, Chadema kilipata
 kura
 67, CCM 20 na CUF 9, Kituo A3 Chadema kura 57, CCM 25 na CUF 7.


Katika kituo cha B4, Chadema kura 54, CCM 30 na CUF 9, B3 Chadema 54, CCM 
15 na 
CUF 9, wakati B2 Chadema kilipata kura 73, CCM 9 na CUF 4 na kituo A2, Chadema 69,
 CCM 21 na CUF 8.
Kituo cha A1, Chadema kura 60, CCM 15 na CUF 11 na B6 Chadema kura 41, CCM 21 
na CUF
 kura 9.

Katika kituo cha B5, Chadema kilipata kura 50, CCM 22 na CUF 10.
Katika kituo cha AICC Nursery School, kituo kidogo cha A2 Chadema kura 58, CCM 
18 na 
CUF 17, A4 Chadema kura 62, CCM 22 na CUF 6, A3 Chadema 44, CCM 22 na CUF 5, 
E2 Chadema 58, CCM 22 na CUF 4, E3 Chadema 53, CCM 20 na CUF 5.

Aidha, katika kituo cha E4 Chadema 40, CCM 20 na CUF 5, B1 Chadema 57, CCM 
18 na CUF 9, A1 Chadema 60, CCM 24 na CUF 5.

Kituo cha Shule ya Sekondari Kaloleli, A1,Chadema 52, CCM 17, CUF 15 huku katika
 kituo cha A2, Chadema kura 97, CCM  23,  CUF 19 na kituo A3, Chadema 46, CCM 
20 na CUF 20.

Kituo cha A4 Chadema 46, CCM, 16, CUF 16, kituo B1 Chadema 56, CCM 10, CUF 16 
na kituo B2 Chadema 42, CCM 23 na CUF 15.Kituo B3, Chadema 53, CCM 17  na CUF 11,
 kituo B4 Chadema 38 CCM 16 na CUF 13

KATA YA ELERAI
Katika Kituo cha Shule ya  Sekondari Kata ya Elerai, Ofisi ya Katibu Tarafa, pia
 Chadema kimeendelea kuongoza katika matokeo ya awali.Matokeo ya jumla Chadema 
kura 2,047, 
CCM 1,471, CUF 302, CCK 3, na TLP 1. Mshindi ni Mhandisi Jeremiah Mpinga wa Chadema.

Kituo A1, Chadema kura 37, CCM 17, CUF 3, TLP na CCK 0. Kituo A2, Chadema kilipata 
kura 28, CCM 13, CUF 2, CCK na TLP 0.Kituo A3, Chadema kura 31, CCM 19, CUF 2, CCK 
na TLP 0 huku katika kituo A4 , Chadema 21, CCM 12, CUF 6 , TLP na CCK 0.

Vituo vingine katika kata hiyo ni pamoja na B1 ambacho Chadema waliongoza kwa kura 
42, CCM 15, CCK na TLP 0 huku katika kituo C1, Chadema 42, CCM 15, CCK na TLP 0.
Kwa upande wa kituo cha C2, CCK 0, CCM 12, Chadema 35, CUF 3 na TLP 0, Kituo kingine 
cha Katibu Tarafa Ofisi, CCM kilipata kura 26, Chadema 25 na CUF huku cha B1 Chadema 
wakijipatia kura 43, CCM 23, CUF 5.

 Kituo B2, Chadema 34, CCM 24, CUF na TLP 0, kituo B3  CCM kura 26, Chadema 32, CUF 3,
 kituo cha Shule ya Msingi Burka B2, CCM ilinyakua kura 31, Chadema 30, CUF 2 na kituo
 B3, CCM ikipata kura 41, Chadema 43, CUF 5 wakati CCK na TLP wakiambulia patupu.

Aidha katika kituo hicho cha Shule ya Msingi Burka,B4 CCM ilipata 32, Chadema 28, CUF 3,
 TLP na CCK 0, vituo vya C1, CCM kura 26, Chadema 43, CUF 5 na kile cha C2, CCK 0, CCM 31, Chadema 43, CUF 7 na TLP 0.

KATA YA KIMANDOLU
Katika Kata ya Kimandolu kwenye kituo Shule ya Msingi Suye, CCM na Chadema 
ndivyo pekee vilisimamisha wagombea.

Katika kituo cha A1, CCM ilipata kura 15, Chadema 47, A2  CCM 24, Chadema 39, kituo
 A3 CCM 14, Chadema 35,  kituo B1 CCM 25, Chadema 56,  kituo B2 CCM 25, Chadema 48, 
kituo C2 CCM 30, Chadema 39 na kituo C1 CCM 11, Chadema 48.

Kituo cha ofisi ya Kata ya  Kimandolu, kituo A1 Chadema ilipata kura 97, CCM 22,  kituo 
A2  Chadema 88, CCM 29, kituo A3 Chadema 81, CCM 31, kituo A5 Chadema 90, CCM 41, 
kituo A6 Chadema 87, CCM 28, kituo A7 Chadema 70, CCM 35,  kituo B1 Chadema 84, CCM 27 
na kituo B2 Chadema 82, CCM 27.

Kituo B3 Chadema 78, CCM 37, kituo B4 Chadema 87, CCM 36, kituo cha B5 Chadema 69, 
CCM 23, kituo C1 Chadema 97, CCM 28, kituo C2 Chadema 103,CCM 21, kituo C3 Chadema 79, 
CCM 32, kituo C4 Chadema 84 CCM 42 na kituo C5 Chadema 87 CCM 41.

Kituo cha Shule ya Msingi Kimandolu kwenye kituo A1 CCM ilipata kura 34, Chadema 64, kituo 
B2 CCM 26, Chadema 66, kituo B4 CCM 37, Chadema 74, kituo A5 CCM 48, Chadema 58, kituo 
A3 CCM 48, Chadema 53, kituo B5 CCM 24, Chadema 65, kituo C1 CCM 27, Chadema 74, kituo C3
 CCM 36, Chadema 64, kituo C5 CCM 31, Chadema 78, kituo A2 CCM 27, Chadema 87, kituo A4 
CCM 33, Chadema 57, kituo B2 CCM 30, Chadema 77 na kituo C2 CCM 30,Chadema 65.

KATA YA THEMI
Katika kata hiyo iliyokuwa na vituo 12, Chadema ilinyakua jumla ya kura 674, CCM 326 na
 CUF 307. Waliojiandikisha walikuwa 6,387, waliopiga kura 1,319, kura halali 1,307 
ambapo zilizoharibika 12, kwa mujibu wa Msimamizi wa Uchaguzi wa kata hiyo, Eveka Mboya 
ambaye pia alimtangaza mshindi kuwa ni Kinabo Edmund wa Chadema.

Matokeo kwa baadhi ya vituo yalionyesha kuwa katika Kituo cha Ofisi ya Mtendaji wa  Kata 
ya Themi, CCM  9, Chadema 36, CUF 0, kituo A2 CCM kura 13, CUF 3 na Chadema 23, kituo 
cha A3 , Chadema 33, CCM 16, CUF 2 na katika kituo A1, CCM ikijipatia kura  44, CUF 1, 
Chadema 53.Katika kituo A2, CCM 29, Chadema 57 na CUF 4 huku kile cha A3 CCM ikijipatia 
kura 23, Chadema 44 na CUF kikiambulia 0.

Kata ya Themi ilikuwa na vituo 12 ambapo hadi tunakwenda mitamboni matokeo ya vituo 
sita yalikuwa yamepatikana huku matokeo ya vituo vingine yakiendelea kuhesabiwa.


No comments: