Saturday, March 27, 2010

JKazindua ujenzi wa machinjio ya kisasa


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa pamoja na waziri wa Maendeleo ya Mifugo na uvuvi Dr.John Pombe Magufuli(wapili kushoto),Mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama Jenerali Davis Mwamunyange(wanne kushoto) na Mwenyekiti wa Bodi ya Ranchi za taifa Bwana Salum Shamte(kushoto) muda mfupi baada ya kuweka jiwe la msingi katika machinjio ya kisasa huko ruvu mkoa wa Pwani unaofanywa na shirika kla SUMA JKT leo asubuhi.

Wataalamu wa ujenzi kutoka katika shirika la SUMA JKT wakimpa Rais Jakaya Mrisho Kikwete maelezo ya maendeleo ya ujenzi wa machinjio ya kisasa unaofanywa na shirika hilo wakati Rais alipokuwa akikagua ujenzi huo muda mfupi baada ya kuweka jiwe la msingi katika machinjio hayo leo asubuhi.
(Picha na Fredy Maro)

No comments: