Tuesday, March 16, 2010

Mabalozi wapya: Mwanaidi Majaar - Marekani


Katika taarifa yake ya leo ya redio, TBC1 inatangaza kuwa Raisi Jakaya Mrisho Kikwete amemteua balozi Mwanaidi Sinare-Maajar kuwa balozi mpya wa Tanzania nchini Marekani kuchukua nafasi ya balozi Ombeni Sefue.

Balozi huyo anakuwa mwanamke wa kwanza wa Tanzania kushika nafasi hiyo ya ubalozi nchini Marekani. Kabla ya hapo, balozi Majaar alikuwa akishikilia wadhifa kama huo huko nchini Uingereza.

Taarifa hiyo pia inasema kuwa balozi mpya wa Tanzania nchini Afrika Kusini ni bi Radhia Mtengeti-Msuya na anaishika nafasi hiyo baada ya aliyekuwa balozi katika nafasi hiyo, Emanuel Mwambulukutu, kustaafu.
SOURCE: http://haki-hakingowi.blogspot.com/

No comments:

CHEREKO ZATAWALA BANDA LA REA KATIKA MAONESHO YA TEKNOLOJIA YA MADINI GEITA

Furaha na shangwe (chereko) zimetawala katika Banda la Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wakati wananchi walipofurika kununua majiko ya gesi ...