Tuesday, March 16, 2010

Mabalozi wapya: Mwanaidi Majaar - Marekani


Katika taarifa yake ya leo ya redio, TBC1 inatangaza kuwa Raisi Jakaya Mrisho Kikwete amemteua balozi Mwanaidi Sinare-Maajar kuwa balozi mpya wa Tanzania nchini Marekani kuchukua nafasi ya balozi Ombeni Sefue.

Balozi huyo anakuwa mwanamke wa kwanza wa Tanzania kushika nafasi hiyo ya ubalozi nchini Marekani. Kabla ya hapo, balozi Majaar alikuwa akishikilia wadhifa kama huo huko nchini Uingereza.

Taarifa hiyo pia inasema kuwa balozi mpya wa Tanzania nchini Afrika Kusini ni bi Radhia Mtengeti-Msuya na anaishika nafasi hiyo baada ya aliyekuwa balozi katika nafasi hiyo, Emanuel Mwambulukutu, kustaafu.
SOURCE: http://haki-hakingowi.blogspot.com/

No comments:

WIZARA YA AFYA YAOMBA SH. TRILIONI 1.8 BAJETI YA 2026/2027

  Wizara ya Afya imeomba kuidhinishiwa jumla ya Shilingi trilioni 1.8 kwa mwaka wa fedha 2026/2027 kwa ajili ya kuendelea kuboresha huduma z...