Tuesday, March 16, 2010

Mabalozi wapya: Mwanaidi Majaar - Marekani


Katika taarifa yake ya leo ya redio, TBC1 inatangaza kuwa Raisi Jakaya Mrisho Kikwete amemteua balozi Mwanaidi Sinare-Maajar kuwa balozi mpya wa Tanzania nchini Marekani kuchukua nafasi ya balozi Ombeni Sefue.

Balozi huyo anakuwa mwanamke wa kwanza wa Tanzania kushika nafasi hiyo ya ubalozi nchini Marekani. Kabla ya hapo, balozi Majaar alikuwa akishikilia wadhifa kama huo huko nchini Uingereza.

Taarifa hiyo pia inasema kuwa balozi mpya wa Tanzania nchini Afrika Kusini ni bi Radhia Mtengeti-Msuya na anaishika nafasi hiyo baada ya aliyekuwa balozi katika nafasi hiyo, Emanuel Mwambulukutu, kustaafu.
SOURCE: http://haki-hakingowi.blogspot.com/

No comments:

RAIS DKT. MWINYI: TUWALEE VIJANA KATIKA MAADILI, TUDUMISHE AMANI KUELEKEA UCHAGUZI

Zanzibar, 11 Julai 2025 — Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ametoa wito wa kitaifa kwa ...