Friday, March 19, 2010

Maaskofu wasaidizi waapishwa



Newly ordained Dar es Salaam Arch-diocese auxiliary bishops Eusebius Nzigilwa (left) and Salutarus Libena bless the Catholic faith followers and invited guests during their consecration mass at Msimbazi parish yesterday. PHOTO/SALHIM SHAO

XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX

Mamia washuhudia kuwekwa wakfu maaskofu wasaidizi
Fidelis Butahe

VIONGOZI mbalimbali wa serikali, dini na vyama vya siasa wakiongozwa na Rais mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa jana walihudhuria ibada ya kuwekwa wakfu, maoskofu Salutarus Libena na Eusebius Nzigilwa.

Maoskfu hao walisimikwa rasmi jana na Askofu Mkuu wa Jimbo la Dar es Salaam, Mwadhama Kardinali Polycarp Pengo, tayari kuwa wasaidizi wake katika Jimbo la Kanisa Katoliki la Dar es Salaam.

Baadhi ya viongozi waliohudhuria ibada hiyo ni pamoja na Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu wa Bunge), Philip Marmo aliyemwakilisha Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.

Hali kadhalika, Jaji Mkuu wa Tanzania Agustino Ramadhani, Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, John Magufuli, Spika wa Bunge, Samwel Sitta, Waziri mstaafu George Kahama.

Viongozi wengine ni , Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia na Askofu Mkuu wa Kanisa la KKKT, Alex Malasusa.

Maaskofu hao kutoka majimbo ya Mahenge na Dar es Salaam walitangaza kuwa wasaidizi wa Askofu Mkuu wa Jimbo la Dar es Salaam Januari 28 mwaka huu.

Hatua hiyo ilifanywa na Baba Mtakatifu Benedict wa XVI baada ya kuombwa na Kardinali Pengo, kufuatia kutokuwa na wasaidizi.

Akitoa shukrani na salamu kwa watu mbalimbali waliohudhuria ibada hiyo, Kardinali Pengo alisema Jimbo Kuu la Dar es Salaam, sasa litakuwa na wasaidizi wawili.

Alisema kwa msingi huo ameamua kuligawa katika sehemu mbili ambapo Askofu Eusebius Nzigilwa atakuwa msimamizi na mzungumzaji mkuu wa makanisa yote yaliyoko upande wa kulia wa Kanisa la Mtakatifu Joseph kuelekea mkoani Morogoro kwa kupitia Barabara ya Morogoro.

“Askofu Salutarus Libena yeye atakuwa msemaji na msimamizi mkuu wa makanisa yote yaliyopo upande wa kushoto kama unatokea kanisa la Mtakatifu Joseph kuelekea Morogoro kwa kutumia Barabara ya Morogoro”

Huku akizitaja Parokia zitakazokuwa chini ya wasaidizi wake Kardinali Pengo alisema Askofu Eusebius Nzigilwa atakuwa akisimamia Kurugenzi ya Fedha, Elimu, Afya na Caltas huku askofu Salutarus Libena akisimamia Kurugenzi ya Litulujia, Mawasiliano na Vijana.

Pia alizitaja Kurugenzi zitakazokuwa chini yake kuwa ni za Utoto Mtakatifu, Wanaume Katoliki, Wawata, Mahakama ya Kanisa, Halmashauri ya Walei Jimbo na Mapadri.

"Maaskafo hawa watakuwa na ofisi pembeni ya ofisi yangu, lakini askofu Salutarus Libena atakaa na mimi kule Kurasini na Eusebius Nzigilwa atakaa kule Osterbay kwenye nyumba ya askofu msaidizi wa zamani wa Jimbo la Dar es Salaam,” alisema.

Mara baada ya Kardinali Pengo kusoma sala wa wakfu aliwatangaza maaskofu hao rasmi na kuwapaka mafuta, kuwavalisha pete, kofia na baadaye kuwapa fimbo kama alama ya huduma ya kiuchungaji.

Hatua hiyo ilizua shangwe kutoka kwa ndugu wa maaskofu hao na kusababisha mtoa ratiba ya ibada hiyo kuwataka ndugu hao kutulia kwa kuwa ibada ilikuwa ikiendelea.

Akizungumza kwa niaba ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda ambaye alialikwa kama mgeni rasmi kutoka serikali, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera na Uratibu wa Bunge, Philip Marmo alisema serikali inafahamu mchango wa Kanisa Katoliki si tu katika utoaji wa huduma za jamii kama elimu, afya bali hata katika upande wa kuwajenga watu kimaadili

1 comment:

Fita Lutonja said...

This is good work from my news editor. Generally I missed U so much but i know that one day one time we gonna meet. Good! and have nice work and God bless U including Chief Makunga whom I appreciate so much.