Habari tulizozipata hivi punde zinasema kuwa 24 wamekufa papo hapo na wengine 56 wamejeruhiwa katika ajali ya basi iliyotokea jana jioni eneo la mpaka kati ya Nzega na Igunga mkoani Tabora.
Ajali hiyo imetokea majira ya saa 10: 15 jioni katika vijiji vya Kitangili na Migua baada ya basi aina ya Scania lililokuwa likitoka Arusha kwenda Mwanza kupinduka.
Waliokufa ni wanaume 14, wanawake sita na watoto wanne huku majeruhi ni wanaume 35, wanawake kumi na watoto 7 huku majeruhi wanne wamepelekwa katika Hospitali ya Bungando mkoani Mwanza kwa matibabu zaidi.
Mganga wa wilaya ya Nzega, Dk John Mwombeki alisema maiti pamoja na majeruhi hao wapo katika hospitali ya Nzega. Taarifa zaidi tutawaleteeni baadaye.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
RAIS SAMIA ATEMBELEA MABANDA YA MAONESHO YA NANENANE JIJINI DODOMA
Tarehe 8 Agosti 2025, viwanja vya Nzuguni Jijini Dodoma vilikua kitovu cha shughuli nyingi wakati wa Maonesho ya Kitaifa na Kimataifa ya Nan...

-
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu na timu ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa akiwa katika ...
-
NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA PSLE-2014 EXAMINATION RESULTS ARUSHA DAR ES SALAAM DODOMA IRINGA KAGERA KIGOMA ...
-
Mwanamuziki toka Jamhuri ya KIdemokrasia ya Kongo, Mbilia Bel akitumbuiza katika viwanja vya bunge mjini Dodoma jana. Picha na Jube Tranquil...
No comments:
Post a Comment