Friday, January 15, 2010

Rais Kikwete ahudhuria sherehe za kuapishwa kwa Rais Guebuza Msumbiji!!


Rais Armando Emilio Guebuza wa Msumbiji akinyoosha juu katiba ya Msumbiji muda mfupi baada ya kula kiapo kuendelea kuingoza nchi hiyo kwa muhula wa pili wa Urais katika sherehe zilizofanyika katika mji mkuu wa nchi hiyo Maputo.Kushoto ni Rais wa Mahakama ya katiba wa Msumbiji Luis Mondlane aliyemwapisha Rais Guebuza.

Rais Armando Emilio Guebuza wa Msumbiji akila kiapo cha Urais Mbele ya Rais wa Mahakama ya Katiba ya Msumbiji Jaji Luis Mondlane katika viwanja vya Uhuru jijini Maputo Msumbiji.

Rais Jacob Zuma wa Afrika ya Kusini akisisitiza jambo wakati akizungumza na Rais Jakaya Mrisho Kikwete na mwenyeji wao Rais Armando Emilio Guebuza wa Msumbiji katika ikulu ya Mjini Maputo muda mfupi baada ya Rais Guebuza kuapishwa kuendelea kuingoza nchi hiyo katika muhula wa pili wa urais.

Rais Jacob Zuma wa Afrika ya Kusini akiteta jambo na Rais Jakaya Mrisho Kikwete wakati wa sherere za kuapishwa kwa Rais Armando Emilio Guebuza kendelea kuingoza Msumbiji katika muhula wa pili wa Urais jijini Maputo.Katikati ni Mke wa Rais Mama Salma Kikwete(picha na Freddy Maro)

No comments: