Monday, January 11, 2010

Mchungaji Mtikila atupwa rumande



MWENYEKITI wa DP, Mchungaji Christopher Mtikila atalazimika kukaa rumande kwa siku kadhaa baada ya hakimu kumfutia dhamana katika kesi yake ya kumkashifu Rais Jakaya Kikwete kutokana na kushindwa kufika mahakamani mara kadhaa.

Hakimu mkazi wa Mahakama ya Kisutu, Waliarwande Lema alifikia uamuzi wa kumuweka rumande baada ya mchungaji huyo kushindwa tena kufika mahakamani na baadaye kudai kuwa alikuwa akimfuatilia daktari aliyemfanyia upasuaji baada ya kuumwa na nyoka.

"Sababu hizo, si za kutiliwa maanani na ili kutoendeleza tabia hiyo nakufutia dhamana," alisema Hakimu Lema baada ya kusikiliza utetezi wa Mtikila ambaye amewahi kugombea urais mara tatu kwa tiketi ya DP (Democtratic Party)

No comments:

NAIBU WAZIRI WA FEDHA AMWAKILISHA WAZIRI WA FEDHA KATIKA KONGAMANO LA 16 LA MWAKA LA WATAALAM WA UNUNUZI NA UGAVI – ARUSHA

Naibu Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Mhandisi Mshamu Ali Munde, amemwakilisha Waziri wa Fedha katika ufunguzi wa Kongamano la 16 la Mwaka la Wa...