Tuesday, January 12, 2010

KAMATI NDOGO YA EALA YAKUTANA ARUSHA



Kamati ndogo ya uongozi ya Bunge la Afrika Mashariki (EALA) inakaa mjini
Arusha chini ya mwenyekiti wake Abdullah Mwinyi kujadili ripoti ya
mafanikio ya miaka miwili na nusu tangu kuapishwa kwa Bunge la Pili.

Mwinyi alisema kua baada ya kujadili taarifa hizo watapeleka mapendekezo
yao katika kikao cha Kamati kuu ya uongozi chini ya Spika wa Bunge hilo
kitakachokaa mwishoni mwa wiki hii.

Baadae kamatikuu hiyo itapeleka mapendekezo yake katika kikao cha tatu cha
bunge hilo kitakacho kaa kitika nchi ya Uganda, Kampala mwezi wa pili mwaka
huu.

Kamati hiyo inaundwa na Wajumbe kutoka nchi zote tano Kenya, Tanzania,
Uganda, Rwanda na Burundi ambao ni wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

No comments:

KIKWETE ATEULIWA KUWA MWAKILISHI WA NGAZI YA JUU WA MWENYEKITI WA KAMISHENI YA AU

Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika (AUC), Mhe. Mahmoud Ali Youssouf, amemteua Rais Mstaafu wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Ki...