Tuesday, January 12, 2010

KAMATI NDOGO YA EALA YAKUTANA ARUSHA



Kamati ndogo ya uongozi ya Bunge la Afrika Mashariki (EALA) inakaa mjini
Arusha chini ya mwenyekiti wake Abdullah Mwinyi kujadili ripoti ya
mafanikio ya miaka miwili na nusu tangu kuapishwa kwa Bunge la Pili.

Mwinyi alisema kua baada ya kujadili taarifa hizo watapeleka mapendekezo
yao katika kikao cha Kamati kuu ya uongozi chini ya Spika wa Bunge hilo
kitakachokaa mwishoni mwa wiki hii.

Baadae kamatikuu hiyo itapeleka mapendekezo yake katika kikao cha tatu cha
bunge hilo kitakacho kaa kitika nchi ya Uganda, Kampala mwezi wa pili mwaka
huu.

Kamati hiyo inaundwa na Wajumbe kutoka nchi zote tano Kenya, Tanzania,
Uganda, Rwanda na Burundi ambao ni wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

No comments:

NAIBU WAZIRI WA FEDHA AMWAKILISHA WAZIRI WA FEDHA KATIKA KONGAMANO LA 16 LA MWAKA LA WATAALAM WA UNUNUZI NA UGAVI – ARUSHA

Naibu Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Mhandisi Mshamu Ali Munde, amemwakilisha Waziri wa Fedha katika ufunguzi wa Kongamano la 16 la Mwaka la Wa...