Sunday, June 15, 2008

Stars yaishangaza Cameroon



Rais Kikwete akiongoza maelfu ya wadau kuishangilia taifa stars mara baada ya kipyenga cha mwisho kulia. japokuwa kila mmoja alitamani kuchukua pointi zote tatu muhimu, lakini hako kamoja ka sare na moja ya timu kali kuliko zote barani afrika si haba ati. wadau mwasemaje?




LICHA ya kuwa na wachezaji mahiri na wanaocheza klabu kubwa za Ulaya, Cameroon imepunguzwa kasi na kuduwazwa na timu ya taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' katika mchezo wa kufuzu kucheza fainali za Kombe la Dunia na Mataifa ya Afrika mwaka 2010.
Ikiwa na majina makubwa kama Samuel Eto'o wa Barcelona, kiungo wa Arsenal Alexander Song na Geremi Njitap wa Newcastle, Cameroon ilijikuta ikipigiwa pasi mfululizo na vijana wa Marcio Maximo katika mechi hiyo iliyofanyika jana kwenye Uwanja Mkuu wa Tanzania na kushuhudia matokeo ya suluhu na kosa kosa kadhaa.
Matokeo hayo yameifanya Cameroon kuwa na pointi saba, huku Taifa Stars ikiwa na pointi mbili, lakini ina matumaini ya nafasi ya pili iwapo itazifunga timu za Cape Verde na Mauritius katika mechi za marudiano.
Cameroon ambao waliingia uwanjani na kuanza kucheza soka la mipango zaidi walijikuta wakipigwa na butwaa baada ya mipango yao kutofanikiwa na kujikuta wakipata upinzani mkali kutoka kwa vijana hao wa Maximo. Picha za Mdau Mpoki Bukuku.

No comments: