Wednesday, June 11, 2008

MAwaziri wafa ajalini

Lorna Laboso1961 — 2008.
Kipkalya Kones: 1952 — 2008.

Ms Aurelia Langat, a sister-in-law of Assistant minister Lorna Laboso overcome by grief on receiving the news of her death

Prime Minister Raila Odinga consoles the family of Roads Minister Kipkalya Kones at their home in Nairobi, on Tues


NDEGE ndogo ya abiria aina ya Cessna 210 imeanguka nchini Kenya na kusababisha vifo vya watu wanne, akiwemo Waziri wa Barabara Kipkalya Kones na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Lorna Laboso.

Ajali hiyo ambayo ilitokea kilomita 120 (maili 75), Magharibi mwa jiji la Nairobi pia imesababisha kifo cha Ofisa wa Polisi, Kenneth Bett na Rubani Schner Christopher.

Vifo vya mawaziri hao kutoka Chama cha Orange Democratic Movement (ODM), vimefanya hadi sasa chama hicho kupoteza wabunge wanne tangu kufanyika Uchaguzi Mkuu wa Desemba mwaka jana ambao ulifuatiwa na ghasia kabla ya mkataba wa amani kusainiwa Februari 28 mwaka huu.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka gazeti la Daily Nation na Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC) na Shirika la Habari la Uingereza (Reuters), ndege hiyo iliyokuwa na namba 5Y BVE ilianguka katika Wilaya ya Narok.

Taarifa kutoka gazeti la Daily Nation ambazo zilinukuuu duru za vyombo vya usalama nchini humo, zilisema ndege hiyo ilikuwa ikienda Kericho ndipo ajali ilipotokea mnamo saa 9 alasiri jana. Hebu soma cheki East Africa Standard

No comments: