Habari tulizo nazo hivi sasa zinasema kuwa watu wanane amefariki dunia katika ajali ya helikopta ya jeshi la ulinzi iliyokuwa njiani ikitokea Arusha kuelekea Dodoma.
inasemekana abiria wake ambao bado haijathibitishwa kuwa ni raia ama askari walikuwa wanatokea arusha kwenye mkutano wa sullivan.
inasemekana waliokufa ni abiria sita na marubani wawili wa helikopta hiyo. habari kutoka kikosi cha anga ama airwing Ukonga imethibitisha habari hiyo na tayari ndege imeenda eneo la tukio na kwamba taarifa kamili itatolewa baadaye.
Taarifa iliyotolewa na Kitengo cha Habari Makao Makuu ya Jeshi ilisema helkopita hiyo ya JWTZ yenye namba 9507 iliyokuwa inarejea Dar es Salaam, ilianguka saa 6.40 mchana katika eneo la Oljoro nje kidogo ya Jiji la Arusha.
Taarifa hiyo ilitaja waliofariki katika ajali hiyo ni marubani wawili, mafundi ndege wawili na abiria wawili. Ndege hiyo ilikuwa kati ya ndege mbili zilizokuwa zikitumika kwa shughuli za ulinzi, wakati wa mkutano wa Sullivan.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
KAMISHNA WA UHIFADHI TANAPA AFANYA ZIARA YA KIKAZI KITUO CHA MALIKALE – MTWA MKWAWA, IHINGA, IRINGA
Kamishna wa Uhifadhi wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA), CPA Musa Nassoro Kuji , amefanya ziara ya kikazi katika Kituo cha Malikale ch...
-
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu na timu ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa akiwa katika ...
-
Mwanamuziki toka Jamhuri ya KIdemokrasia ya Kongo, Mbilia Bel akitumbuiza katika viwanja vya bunge mjini Dodoma jana. Picha na Jube Tranquil...
-
(Picha na Yahya Charahani) Katika kijiji cha Mwanjoro, wilayani Meatu – Shinyanga, maisha bado yanapumulia kwenye nyumba za udongo na mapaa...
No comments:
Post a Comment