Habari tulizo nazo hivi sasa zinasema kuwa watu wanane amefariki dunia katika ajali ya helikopta ya jeshi la ulinzi iliyokuwa njiani ikitokea Arusha kuelekea Dodoma.
inasemekana abiria wake ambao bado haijathibitishwa kuwa ni raia ama askari walikuwa wanatokea arusha kwenye mkutano wa sullivan.
inasemekana waliokufa ni abiria sita na marubani wawili wa helikopta hiyo. habari kutoka kikosi cha anga ama airwing Ukonga imethibitisha habari hiyo na tayari ndege imeenda eneo la tukio na kwamba taarifa kamili itatolewa baadaye.
Taarifa iliyotolewa na Kitengo cha Habari Makao Makuu ya Jeshi ilisema helkopita hiyo ya JWTZ yenye namba 9507 iliyokuwa inarejea Dar es Salaam, ilianguka saa 6.40 mchana katika eneo la Oljoro nje kidogo ya Jiji la Arusha.
Taarifa hiyo ilitaja waliofariki katika ajali hiyo ni marubani wawili, mafundi ndege wawili na abiria wawili. Ndege hiyo ilikuwa kati ya ndege mbili zilizokuwa zikitumika kwa shughuli za ulinzi, wakati wa mkutano wa Sullivan.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Bodi ya Kitaaluma ya Ununuzi na Ugavi (PSPTB), inayofanya kazi chini ya Wizara ya Fedha, imetoa onyo kali kwa watahiniwa wote wa fani ...
-
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu na timu ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa akiwa katika ...
-
Mwanamuziki toka Jamhuri ya KIdemokrasia ya Kongo, Mbilia Bel akitumbuiza katika viwanja vya bunge mjini Dodoma jana. . Picha na Jube Tranqu...
-
Hapa mmoja wa watoto hao akiwa na kijana mwenzake mwenye miaka 18, wote wako sawa lakini yeye hawezi kuzungumza kama watu wa kawaida. Mama S...
No comments:
Post a Comment