Sunday, June 15, 2008

CCM wakaangana


Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM na Mawaziri wakuu wastaafu, Cleopa Msuya (katikati), Fredercick Sumaye (kulia) na Edward Lowassa (kushoto) wakiwa katika mkutano wa wabunge wote wa CCM na wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM ulioongozwa na Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete kwenye ukumbi wa African Dream mjini Dodoma Juni 15,2008.

Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akijiandaa kufungua mkutano wa Wabunge wote wa CCM na wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM uliofanyika kwenye ukumbi wa African Dream, Area D mjini Dodoma Juni 15, 2008.
Viongozi wengine kutoka kushoto ni Spika wa Bunge Samwel Sitta, Makamu Mwemyekiti wa CCM na Rais wa Zanzibar, Aman Karume na kulia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM,Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.



Mwenyekiti wa CCM,Rais, Jakaya Kikwete na viongozi wengine wakiwa kwenye ukumbi wa African Dream, Area D mjini Dodoma kabla ya kuanza kwa mkutano wa wabunge wote wa CCM na wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM juni
15,2008. Viongozi hao kutoka kushoto ni Spika wa Bunge, Samwel Sitta, Katibi Mkuu wa CCM Mstaafu, Rashidi Kawawa, Mamamu Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Zanzibar Aman Karume, Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba na Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Pius Msekwa. (Picha zote na Ofisi ya Waziri Mkuu)

No comments: