Monday, June 16, 2008

Hali si shwari Baktata



WALIOKUWA viongozi waandamizi wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata), wamekutana kujadili hatua ya Mufti wa Tanzania, Sheikh Mkuu Issa bin Shaaban Simba kuwavua uongozi katika mazingira ya kutatanisha.

Viongozi waliovuliwa uongozi ni aliyekuwa Naibu Mufti, Sheikh Abubakar Zubeir, Katibu wa Mufti ambaye na Naibu Katibu wa Baraza la Ulamaa la Bakwata Taifa, Sheikh Abdushakur Omar.

Wengine ni Katibu wa Baraza la Ulamaa, Sheikh Hassan Chizenga, Mwenyekiti wa Halmashauri Kuu Taifa, Sheikh Khamis Mataka na wajumbe wawili wa Baraza la Ulamaa, Sheikh Suleiman Kilemile na Sheikh Hamid Jongo.

Habari zilizopatikana jana zinaeleza kwamba, baadhi ya viongozi hao, kuanzia juzi na jana, wamekuwa wakifanya vikao jijini Dar es Salaam, wakijadili hatua hiyo ya Mufti Simba na hatma yao Bakwata. Habari ya Muhibu Said.

No comments: