Friday, June 20, 2008

Iddi Amin




Kundi zima maigizo likiwa katika kujitangaza leo hii hapa jijini Dar es Salaam Msanii Lumole Matovolwa anayeigiza kama, Iddi Amini-Dadaa akiwa na wenzake walipozungumzia uzinduzi wa mchezo wa kuigizo waliouipa jina la Juliana. Mchezo huo, unatarajiwa kuzinduliwa Juni 26 kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee.

1 comment:

Anonymous said...

Igizo hili linaweza kuzuwa mtafaruku mkubwa sana wa kisiasa kati ya Tanzania na Uganda.

Dhana na waigizaji wa igizo hili vyote havijafanyiwa tathimini ya kina (critical reflection/analysis).

Kwa upande wa dhana (theme), igizo linazungumzia Juliana na jinsi UKIMWI ulivyokuja Tanzania baada ya vita na Uganda. Hii si dhana makini hata kidogo. Si hekima kwa ncho moja kutuhumu nyingine kama chanzo chake cha UKIMWI.

Kwa upande wa waigizaji (characters). Nina hakika atakayemuigiza Idd Amini atamuigiza katika taswira iliyozoeleka (stereotype) juu ya Idd Amini. Taswira ambayo mara nyingi imemsawiri Idd Amini kama mtu katili na mjinga mjinga (mediocre/naive).

Dhana na waigizaji wa mchezo huu unaweza kuwa tusi (insult/offence) kwa Waganda.

BASATA vipi mlilitathimini igizo hili? Taasisi ya Utamaduni Bagamoyo mlishirikishwa katika maandalizi ya igizo hili?

Ni mimi,

Muigizaji wa siku nyingi.