Tuesday, June 24, 2008

Maweeeee Flaviana


"Namshukuru Mungu sijaharibu kwa kweli ingawa wakati mwingine waandishi wa habari huwa wanaandika mambo yasiyokuwa na ukweli ndani yake.Hata hivyo mimi husema pengine hiyo ni moja ya kazi yao.Kimsingi, vyombo vya habari ndio vinavyonyanyua na kuchafua pia.Hivyo ni ngumu sana kuelezea ingawa nina imani hili linafahamika.

Jambo ambalo ningependa kuliweka sawa ni kuhusu kilichotokea siku ya uzinduzi wa upimaji ukimwi pale Mnazi Mmoja.Jamani mimi hamna mtu aliyenilazimisha kwenda pale siku ile. Niliamua mwenyewe na nilikuwa najiamini. Sasa nilisikitika pale nilipozirai(faint) watu wakaandika habari tofauti.Mimi ni binadamu, pale kulikuwa na jua kali na msongamano wa watu mkubwa kiasi kwamba hewa ikawa haitoshi.

Ile ni hali inayoweza kumtokea mtu yeyote.Hivyo basi nakanusha usemi uliovuma eti nilizirai kutokana na hofu ya kupima",Hayo is maneno yangu Wadau, na maneno ya Mlimbwende Flaviana Matata alipofanya mahojiano ya kina na wanja la kaka Jeff kupitia cheki Bongo Celebrity ,ukitaka kufahamu zaidi kuhusu flavi na harakati zake za kimaisha ingia hapo
 

No comments: