Friday, June 13, 2008

Bajeti kwapukwapu



SERIKALI imeshindwa kupunguza bei ya petroli na dizeli katika bajeti yake ya mwaka 2008/2009, badala yake imewabana wavuta sigara na wanywaji wa bia na soda kwa kupandisha kodi ya bidhaa hizo.

Pamoja na kutoongeza ushuru katika bidhaa za petroli, bado wachambuzi wa masuala ya uchumi wanaona hali itaendelea kuwa ngumu katika sekta za uzalishaji na usafirishaji kutokana na kuongezeka kwa kasi bei ya nishati hiyo katika soko la dunia, hivyo wananchi kuendelea kuishi katika hali ngumu katika kipindi cha mwaka huu wa bajeti.

Bajeti hiyo pia imeongeza ushuru wa bidhaa katika huduma za simu za mkononi kutoka asilimia saba ya gharama ya matumizi ya huduma hadi asilimia 10. Kwa mantiki hiyo, gharama za matumizi ya simu zitaongezeka kwa watumiaji.Hebu soma cheki FULL DOCUMENT YA HOTUBA YA BAJETI YA WAZIRI BUNGENI

No comments: