Sunday, June 29, 2008

Mugabe ashinda, aapishwa


RAIS Robert Mugabe wa Zimbabwe, ameshinda na kuapishwa baada ya uchaguzi wa marudio uliofanyika Ijumaa wiki iliyopita, kwa kupata asilimia 85 ya kura zote zilizopigwa.
Afisa Mkuu wa Tume ya Uchaguzi ya Zimbabwe (Zec), Lovemore Sekeramyi, alisema kuwa Mugabe alishinda kwa jumla ya kura 2,150,269 huku Morgan Tsvangirai wa Chama cha Movement for Democratic Change (MDC), ambaye pamoja na kutangaza kujitoa jina lake liliendelea kuachwa kwenye karatasi za kupigia kura, alipata kura 233,000.
Alisema kuwa katika matokeo hayo yaliyotangazwa jana, yalionyesha kuwa Rais Mugabe ameshinda katika majimbo yote 10 nchini humo, kupitia uchaguzi huo ambao alisimama peke yake.

Kwa taarifa zaidi soma
cheki Shirika la Utangazaji la BBC

1 comment:

Anonymous said...

Hello to eνery single one, it's truly a nice for me to go to see this site, it includes valuable Information.

Here is my weblog; bladder disease