Wednesday, September 28, 2016

NMB WAZINDUA CHIPUKIZI AKAUNTI NA PROGRAMU YA SHULE DIRECT JIJINI DAR ES SALAAM LEO


 Mkuu wa shule ya Sekondari ya Benjamin Mkapa, Gebo Lugano akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo wakati wa uzinduzi wa Proramu ya Shule Direct katika shule hiyo  ambayo itawasaidia wanafunzi kujifunza kwa kutumia Mtandao wa www.shule Direct.co.tz ambapo wanafunzi watajisomea masomo yao kupitia mtandao huo.

Wakati huo huo imezinduliwa akaunti ya ya NMB chipukizi akaunti kwaajili ya wanafunzi pamoja watoto wenye umri wa kuanzia miaka 14 kwaajili ya kujiwekea akiba ikiwa mprogramu hiyo imeanzia katika shule ya shule ya Sekondari ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam leo.
Maneja mwandamizi wa amana, huduma za ziada na bima wa Benki ya NMB, Stephen Adil akizungumza na wanafunzi pamoja na wafanyakazi wa benki ya NMB waliohudhulia katika uzinduzi wa programu ya Shule Direct jijini Dar es Salaam leo katika shule ya Sekondari ya Benjamin Mkapa.
 Baadhi ya wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Benjamin Mkapa waliohudhulia katika kuzinduzi wa Shule Direct pamoja na NMB chipukizi akaunti ambapo baadhi ya wanafunzi wamefungua akaunti wakati huo huo.
 Mkurugenzi wa Shule Direct, Faraja Nyarandu akizungumza wakati wa kuzindua Shule Direct ambapo wanafunzi watatembelea mtandao wa www.shuledirect.co.tz kwaajili ya kujifunzia masomo mbalimbali ambapo wanafunzi watatembelea mtandao huo  kwaajili ya kujifunza masomo mbalimbali. 
 Naibu Waziri wa Kazi, Ajira na Vijana, Antony Mavunde akizungumza wakati wa uzinduzi wa Shule Direct kwa wanafunzu wa shule ya Sekondari ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam leo, amewaasa wa wanafunzi kusoma kwa kutumia mtandao wa www.shule.co.tz kwaajili ya kujifunza zaidi masomo yao na si kutembelea mitandao mingine ambayo haihusiana na masomo yao.
Pia amewaasa kujiwekea akiba zao kupitia akaunti ya Chupukizi ya NMB kwa pesa kidogokidogo wanazopewa na wazazi wao ili ziwafaidisha baadae na si kutumia pesa hovyo.
Naibu Waziri wa Kazi, Ajira na Vijana, Antony Mavunde,  Mkurugenzi wa Shule Direct, Faraja Nyarandu,  pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa NMB pamoja na wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Benjamin Mkapa wakiangalia programu ya Shule Direct jinsi inavyofanya kazi.


 Naibu Waziri wa Kazi, Ajira na Vijana, Antony Mavunde,  Mkurugenzi wa Shule Direct, Faraja Nyarandu na wafanyakazi wa NMB wapewa Maelekezo na Mtaalamu wa Kompyuta wa Programu ya Shule Direct, Erick Kondela wakati wa uzinduzi wa Programu ya Shule Direct katika shule ya Sekondari ya Benjamin Mkapa jijini  Dar es Salaam leo. 
Mkurugenzi wa Shule Direct, Faraja Nyarandu akifafanua jambo kwa wafanyakazi wa benki ya NMB na Naibu Waziri wa Kazi, Ajira na Vijana, Antony Mavunde wakati walipotembelea Darasa la Shule Direct katika shule ya Sekondari ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam leo.
 Mtaalamu wa Kompyuta wa Programu ya Shule Direct, Erick Kondela akiwasimamia baadhi ya wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam leo.
 Naibu Waziri wa Kazi, Ajira na Vijana, Antony Mavunde,  Mkurugenzi wa Shule Direct, Faraja Nyarandu wakiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam leo mara baada ya kuzindua programu ya Shule Direct katika shule hiyo.
 Baadhi ya wanafunzi wakipokea zawadi baada ya kujibu maswali vizuri.
Picha ya Pamoja  baada ya kupata zawadi.

Baadhi ya wanafunzi wakifungua akaunti ya chupukizi ya NMB jijini Dar es Salaam leo

No comments: