Saturday, September 24, 2016

Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa mgeni rasmi kesho Uwanja wa Taifa katika mechi ya kuchangisha fedha kwa ajili ya waathirika wa Tetemeko Kagera

nge2
Mwenyekiti wa Bunge Sports Club  Mhe. William Ngeleja akizungumza na waandishi wa Habari(hawapo pichani) kuhusu mechi ya kesho kati ya wabunge mashabiki wa Simba na Yanga na Wasanii wa Bongo Flava na Bongo Movies katika  Uwanja wa Taifa na kutangaza kuwa mgeni rasmi katika mechi hiyo atakuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mhe Kassim Majaliwa.
nge3
Mwenyekiti wa Bunge Sports Club Mhe. William Ngeleja akionesha moja ya kikombe kwa waandishi wa Habari(hawapo pichani) kitakachotolewa kwa mshindi katika mechi ya kesho kati ya wabunge mashabiki wa Simba na Yanga na Wasanii wa Bongo Flava na Bongo Movies katika  Uwanja wa Taifa.
nge4
Mwakilishi wa wasanii wa Bongo Movie Bw.William Mtitu akizungumza kuhusu maandalizi ya timu yao kabla ya mchezo wao wa kesho na wasanii wa Bongo Flava utakaofanyika katika Uwanja wa Taifa kwa dhumuni la kuchangisha fedha kwaajili ya waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera.
nge5
Mwakilishi kutoka Mwananchi Communications LTD Bw. Francis Nanai akizungumzia mchango wao walioutoa wa kutoa taarifa kwa watanzania kuhusu hali ilivyo mkoani Kagera na kutoa nafasi kwa makampuni yatakayojotokeza kufanya harambee kuwasaidia waathirika wa tetemeko watatoa matangazo bure kwa ajili yao katika vyombo vyao vya habari.
nge6
Mwakilishi kutoka Shirika la Bima ya Afya Taifa NHIF Bw. Baraka Maduhu akitoa ufafanuzi kuhusu huduma za kiafya zitazotolewa kwa wachezaji na wananchi kwa ujumla kesho katika mchezo kati ya wabunge mashabiki wa Simba na Yanga Wasanii wa Bongo Flava na Bongo Movies.
nge7
Mwenyekiti wa Kamati ya Michezo ya Bunge Mhe. William Ngeleja akipokea hundi ya shilling million kumi kutoka kwa Mwakilishi wa Mwananchi Communications LTD Bw. Francis Nanai kwa ajili ya msaada kwa msadaa kwa waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera.
nge8
Mwenyekiti wa Kamati ya Michezo ya Bunge Mhe. William Ngeleja akipokea hundi ya shilling millioni tano kutoka kwa  Mwakilishi wa Jubilee Insurance Bi. Elieth kileo kwa ajili ya msaada kwa msadaa kwa waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera.
nge9
Mwenyekiti wa Kamati ya Michezo ya Bunge Mhe. William Ngeleja akipokea hundi ya shilling millioni tano kutoka kwa  Mwakilishi wa Jubilee Insurance Bi. Elieth kileo kwa ajili ya msaada kwa msadaa kwa waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera.
nge10
Baadhi ya waandishi wa habari wakifatilia mkutano huo.
nge11
Mwenyekiti wa Kamati ya Michezo ya Bunge Mhe. William Ngeleja na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo kutoka Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Alex Nkenyenge wakiwa katika picha ya pamoja na wabunge, wasanii wa bongo movie na bongo flava, wawakilishi wa Mwananchi Communications Ltd, Jubilee Insurance,Shirika la Taifa la Bima ya Afya na Selcom Tanzania mara baada ya mkutano wa kuhamasisha wananchi kushiriki kuchangia waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera kupitia michezo.
(Picha Zote na Raymond Mushumbusi WHUSM.)  

No comments: