Tuesday, September 06, 2016

RAIS MAGUFULI ATOA SIKU 7 KWA WAPANGAJI WOTE SERIKALINI WANAODAIWA NA NHC WALIPE

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu akiagana na  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk John Pombe Magufuli baada ya kuhutubia alipotembelea na kuongea na wakaazi wa  Magomeni Kota wilaya ya Kinondoni  jijini Dar es salaam leo Septemba 6, 2016
 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu   akinyanyuka juu baada ya kupongezwa kwa utendaji wake bora  na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt John Pombe Magufuli wakati alipotembelea na kuongea na wakaazi wa  Magomeni Kota wilaya ya Kinondoni  jijini Dar es salaam leo Septemba 6, 2016.

 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu na watendaji wengine wa Wizara ya Ardhi, Nyyumba na Maendeleo ya Makazi pamoja na Wilaya ya Kinondoni wakimsubiri Rais Magufuli kuwasili katika eneo hilo.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk John Pombe Magufuli akiongozana na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuelekea katika eneo la makazi ya Magomeni.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk John Pombe Magufuli akiongozana na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Vangimembe Lukuvi kuelekea katika eneo la makazi ya Magomeni.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk John Pombe Magufuli akitia saini kwenye kitabu cha wageni huku Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Vangimembe Lukuvi wakishuhudia.

 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu akijadiliana jambo na  Mbunge wa Kinondoni Maulid Mtulia.

                                            &&&&&&&&&&&&&&&&&&


Rais John Pombe Magufuli ametoa siku saba kwa wapangaji wote serikalini wanaodaiwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kulipa madeni yao, pamoja na kutoa agizo kwa viongozi wa shirika hilo kuwatolea vitu nje watakaoshindwa kulipa madeni yao kwa wakati.

Rais Magufuli ametoa agizo hilo leo jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na waliokuwa wakazi wa Magomeni Kota.

“Wapangaji wote lazima walipe madeni yao, natoa agizo leo wapangaji wote serikalini wanaodaiwa na NHC ndani ya siku saba wawe wameshalipa madeni yao, ” amesema.

Ameongeza kuwa “Wasipolipa endeleeni kuwatolea vitu vyao nje kama mlivyotoa vya jamaa, awe wa UKAWA toa nje, wa CCM toa. “

No comments: