Friday, September 09, 2016

TASWIRA MBALIMBALI BUNGENI LEO


Waziri wa Habari, Utaamduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye (MB) akiwaeleza jambo Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini Mhe. Peter Msigwa (Katikati)na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (TAMISEMI) Mhe. George Simbachawene wakati wa kikao cha bunge leo Mjini Dodoma.
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson akiongoza kikao cha bunge leo Mjini Dodoma.
Naibu Waziri Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na Watoto Dkt. Hamis Kigwangalla akijibu swali wakati wa kikao cha bunge na kuahidi kuwa serikali kuendelea kuboresha huduma za afya katika hospitali nchini ikiwemo upatikanaji wa madawa na vifaa tiba.
Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo akiwaeleza wabunge mipango ya serikali kuendelea kushughulikia changamoto za nishati ya umeme nchini hasa katika maeneo ya Lindi na Mtwara
Baadhi ya Wabunge wakiingia katika ukumbi wa bunge mapema leo.
Naibu Waziri Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Ashatu Kijaji akijibu swali kwa wabunge ambapo alisema kuwa Serikali inafanya kila jitihada ya kuwaongezea uwezo katika watendaji wake ili kuendana na mabadiliko ya teknolojia nchini. 


Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Mhe. Charles Tizeba akieleza bungeni leo kuhusu hali ya chakula nchini na kuwahakikishia watanzania kuwa nchi ina utoshelevu wa chakula kwa zaidi ya asilimia 123 kwa mazao ya nafaka na 140.
 PICHA NA HASSAN SILAYO-MAELEZO 

No comments: