Wednesday, June 08, 2016

MAMLAKA YA USAFIRI WA ANGA TANZANIA(TCAA) WATOA MSAADA WA KOMPYUTA KWA WANAFUNZI WENYE ULEMAVU WA AKILI WA SHULE YA MSINGI MTAMBANI BOKO DAR ES SALAAM

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa AngaTanzania.(TCAA), Hamza Johari(kushoto), akikabidhi msaada wa Kompyuta kwa wanafunzi wenye mahitaji maluum wenye ulemavu wa akili wa shule ya Msingi Mtambani, iliyopo Boko jijiniI Dar es salaam. Wanaoshuhudia kutoka kulia ni Mwalimu Mkuu msaidizi wa Shule hiyo Mariana Saso na Mkuu wa Kitengo Maalumu cha Wanafunzi wenye Ulemavu wa akili wa shule hiyo Asaph Maerere.Hafla hiyo imefanyika leo makao makuu ya TCAA Ukonga, Banana.
Mkuu wa Kitengo Maalumu cha Wanafunzi wenye Ulemavu wa akili wa shule ya msingi Mtambani iliyopo Boko jijini Dar es Salaam, Asaph Maerere. akiwa na wanafunzi wake wakiwa wamebeba kompyuta mara baada ya kukabidhiwa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa AngaTanzania.(TCAA), Hamza Johar(hayupo pichani) .
Wanafunzi wenye mahitaji maluum ya ulemavu wa akili wa shule ya Msingi Mtambani, iliyopo Boko jijini Dar es salaam,wakifurahia komputa mara baada ya kukabidhiwa msaada na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa AngaTanzania.(TCAA), Hamza Johar(hayupo pichani)hafla hiyo Hafla hiyo imefanyika leo makao makuu ya TCAA Ukonga, Banana.

No comments: