Friday, February 08, 2008

Waziri Mkuu mpya Mizengo Pinda


Kikao cha bunge kimeanza tena jionni hii mjini dodoma na jina limeshaletwa la Waziri Mkuu mteule. Jina hilo ni Mizengo Kayanza Peter Pinda na sasa tunasubiri wabunge wapige kura, hivi sasa wabunge wanaunga mkono hoja kaanza Hamad Rashid Mohammed kasifia saana akafuata Edward Lowassa naye kasifia ile mbaya, akafuata mama Getrude Mongela amesifu mpaka sijui vipi.

Sasa wanazungumza Anna Abdallah, Zitto Kabwe, John Malechela, Jackson Makwetta na wengineo. Ni mizengo Pinda waziri mkuu mpya!!!!. Picha ni ya mdau Edwin Mjwahuzi aliyepo Dodoma.

No comments:

MHANDISI SEFF AKAGUA UJENZI WA BARABARA ZA UWANJA WA AFCON ARUSHA

#Ataka kazi zikamilike ifikapo Mei 2027 Arusha Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Mhandisi Victor Seff amefa...