MSIMAMIZI Mkuu wa mazungumzo ya pande mbili zinazovutana nchini Kenya, Katibu Mkuu Mstaafu wa Umoja wa Mataifa, Kofi Annan amesimisha mazungumzo ya kutafuta amani.
Akizungumza na vyombo vya habari jana katika Hoteli ya Serena, jijini Nairobi alisema kamati yake imeamua kusimamisha mazungumzo hayo ili kujikita zaidi katika mashauriano na kila upande kwa kina, baada ya kuona hatua ya sasa haizai matunda.
Annan alisema kinachoonekana kwa sasa Kamati hiyo ya usuluhishi inahitaji kukutana na wakuu wa pande hizo mbilI, Rais Mwai Kibaki na Raila Odinga wa ODM kuliko kuendelea kuzungumza na wawakilishi wao, ambao mara kwa mara wamekuwa wakibadilika.
Alisema kwamba mazungumzo hayakusimamishwa bali wanatafuta njia muafaka zaidi, ambayo itakuwa ya kudumu.
"Bado hatujakata tamaa, tunachokitafuta ni suluhu ya kudumu kuliko ilivyo sasa," alisema.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
HESLB NA ADAPT IT ZAINGIA MAKUBALIANO RASMI
Dar es Salaam, Jumatatu, Disemba 08, 2025 Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imeingia katika hatua nyingine ya mageuzi ya k...
-
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu na timu ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa akiwa katika ...
-
Mwanamuziki toka Jamhuri ya KIdemokrasia ya Kongo, Mbilia Bel akitumbuiza katika viwanja vya bunge mjini Dodoma jana. Picha na Jube Tranquil...
-
(Picha na Yahya Charahani) Katika kijiji cha Mwanjoro, wilayani Meatu – Shinyanga, maisha bado yanapumulia kwenye nyumba za udongo na mapaa...
No comments:
Post a Comment