Taarifa tulizo nazo hadi sasa ni kwamba Rais Jakaya Kikwete atatangaza baraza la mawaziri kesho saa nne asubuhi, badala ya leo kutokana na sababu mbalimbali, hali iinayofanya kuwepo kwa hali ya tension kubwa kwa jamii.
Taarifa zisizo rasmi ambazo hazijathibitishwa zinadai kuwa kuahirishwa huko kunatokana na Rais Kikwete kuteua baadhi ya mawaziri kutoka ndani ya chama ambao baadhi wamedaiwa kukataa nyadhifa.
Hata hivyo uvumi mwingine uliokuwa umeenea jana kiasi cha kusababisha tafrani miongoni mwa baadhi ya wananchi na hata wanachama wa vyama vya upinzani na hata CCm ni zille zilizodai kuwa Rais aliteua mawaziri wanne kutoka kambi ya upinzani, ambao walikuwa wapewe nyadhifa katika wizara nyeti.
Lakini taarifa zilizopatikana baadaye zilipingana na taarifa hizo na hakuna hata mmoja aliyethibitisha si viongozi wa vyama vya upinzani na hata wale wa chama cha mapinduzi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
TBC Yawajengea Uwezo Washitiri Uzalishaji wa Vipindi
Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Bw. Gwakisa Mlawa akizungumza wakati wa kufunga Mkutano wa 110 wa wadau wa elimu k...
-
Hapa mmoja wa watoto hao akiwa na kijana mwenzake mwenye miaka 18, wote wako sawa lakini yeye hawezi kuzungumza kama watu wa kawaida. Mama S...
-
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu na timu ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa akiwa katika ...
-
Pascal Mayalla akiwa katika chumba cha wagonjwa Daraja la kwanza katika hospitali ya mkoa wa Dodoma ambako amelazwa kwa matibabu baada ya ku...
No comments:
Post a Comment