Matokeo ya awali ya Uchaguzi Mdogo wa Ubunge katika Jimbo la Kiteto mkoani Manyarayanaonyesha kuwa mgombea bunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Benedict Ole Nangoro ameshinda.
Habari za uhakika zilizokusanywa na gazeti la Tanzania Daima jana usiku baada ya kura kuhesabiwa katika kata zote 15 (ukiacha maeneo machache ambayo alikuwa hajakamilika) yalikuwa yakionyesha kuwa, Nangoro alikuwa amevuna takribani kura 15,000 dhidi ya 11,000 alizokuwa amepata mshindani wake mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Victor Kimesera.
Habari zaidi ambazo Tanzania Daima ilikuwa imezipata majira ya saa 5:00 usiku wa kuamkia leo zilikuwav zikionyesha kuwa Nangoro alikuwa ameshinda katika takribani kata 11 kati ya kata zote 15 zilizokwishakusabiwa huku mpinzani wake akishinda katika kata nne tu.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
TBC Yawajengea Uwezo Washitiri Uzalishaji wa Vipindi
Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Bw. Gwakisa Mlawa akizungumza wakati wa kufunga Mkutano wa 110 wa wadau wa elimu k...
-
Hapa mmoja wa watoto hao akiwa na kijana mwenzake mwenye miaka 18, wote wako sawa lakini yeye hawezi kuzungumza kama watu wa kawaida. Mama S...
-
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu na timu ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa akiwa katika ...
-
Pascal Mayalla akiwa katika chumba cha wagonjwa Daraja la kwanza katika hospitali ya mkoa wa Dodoma ambako amelazwa kwa matibabu baada ya ku...
No comments:
Post a Comment