Matokeo ya awali ya Uchaguzi Mdogo wa Ubunge katika Jimbo la Kiteto mkoani Manyarayanaonyesha kuwa mgombea bunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Benedict Ole Nangoro ameshinda.
Habari za uhakika zilizokusanywa na gazeti la Tanzania Daima jana usiku baada ya kura kuhesabiwa katika kata zote 15 (ukiacha maeneo machache ambayo alikuwa hajakamilika) yalikuwa yakionyesha kuwa, Nangoro alikuwa amevuna takribani kura 15,000 dhidi ya 11,000 alizokuwa amepata mshindani wake mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Victor Kimesera.
Habari zaidi ambazo Tanzania Daima ilikuwa imezipata majira ya saa 5:00 usiku wa kuamkia leo zilikuwav zikionyesha kuwa Nangoro alikuwa ameshinda katika takribani kata 11 kati ya kata zote 15 zilizokwishakusabiwa huku mpinzani wake akishinda katika kata nne tu.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Prof. Mfaransa Aja na Kitabu: Aiambia Dunia Kutalii Tanzania ni Tiba
Na Mwandishi Wetu Paris, Ufaransa Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana, akiwa nchini Ufaransa jana Julai 8, 2025 amek...

-
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu na timu ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa akiwa katika ...
-
NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA PSLE-2014 EXAMINATION RESULTS ARUSHA DAR ES SALAAM DODOMA IRINGA KAGERA KIGOMA ...
-
Mwanamuziki toka Jamhuri ya KIdemokrasia ya Kongo, Mbilia Bel akitumbuiza katika viwanja vya bunge mjini Dodoma jana. Picha na Jube Tranquil...
No comments:
Post a Comment