WAKUU wa Vyuo Vikuu vya Umma nchini wamelaani vurugu zilizofanywa na wanafunzi wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam na kusababisha kifo cha mwanafunzi mmoja na kuazimia kuwa watakaobainika wafukuzwe, wasiruhusiwa kusoma kwenye chuo chote nchini wala kupewa mkopo na serikali.
Sambamba na hilo, wakuu hao wametaka wanafunzi wote watakaopatikana na hatia ya kuhusika na vurugu hizo wasimamishwe kuendelea na chuo na kutoruhusiwa kuendelea na masomo katika chuo chochote cha umma nchini, pamoja na kutolewa katika mpango wa serikali wa kuwakopesha wanafunzi wa vyuo vikuu nchini.
Vurugu hizo zilizofanyika Ijumaa usiku pamoja na mambo mengine wanafunzi hao sehemu ya Mlimani, walivamia nyumba ya Makamu wa Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Rwekaza Mukandala, na kuvunja geti wakishinikiza wapatiwe maji.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
WAZIRI MASAUNI ASHUHUDIA NUSU FAINALI YA KOMBE LA MAPINDUZI ZANZIBAR
Zanzibar — Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Hamad Yussuf Masauni , ameshuhudia mchezo wa kwanza wa nusu fain...
-
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu na timu ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa akiwa katika ...
-
Mwanamuziki toka Jamhuri ya KIdemokrasia ya Kongo, Mbilia Bel akitumbuiza katika viwanja vya bunge mjini Dodoma jana. Picha na Jube Tranquil...
-
Hapa mmoja wa watoto hao akiwa na kijana mwenzake mwenye miaka 18, wote wako sawa lakini yeye hawezi kuzungumza kama watu wa kawaida. Mama S...
No comments:
Post a Comment