Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limemthibitisha Mizengo Kayanza Peter Pinda kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania kuchukua nafasi ya Edward Lowassa aliyejizulu jana.
Mizengo Pinda anakuwa Waziri Mkuu wa 10 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akitanguliwa na JK Nyerere, Rashid Kawawa, Cleopa Msuya, Edward Sokoine, Salim Ahmed Salim, Joseph Warioba, John Malecela, Fredrick Sumaye na Edward Lowassa.
Akitangaza matokeo sasa hivi Spika wa Bunge Samwel Sitta, Pinda amepitishwa rasmi na wabunge kuwa Waziri Mkuu mpya kwa kura 279 za ndio ama asilimia 98.9 wakati kura mbili za hapana na moja imeharibika.
Kuanzia dakika hii mheshimiwa Mizengo Peter Pinda ndiye Waziri Mkuu wetu. Saa tano kamili kesho ataapishwa Ikulu ya Chamwino.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
MMUYA: WANANCHI WANUFAIKE NA UWEKEZAJI WA NHC KUPITIA NYUMBA ZA GHARAMA NAFUU
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Kaspar Mmuya, amekagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa maghala unaotekelezwa na S...
-
Hapa mmoja wa watoto hao akiwa na kijana mwenzake mwenye miaka 18, wote wako sawa lakini yeye hawezi kuzungumza kama watu wa kawaida. Mama S...
-
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu na timu ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa akiwa katika ...
-
Nadhani mtakumbuka kibwagizo maarufu katika TV ambacho kinaimbwa perupe pepero perupe pepero hawa ni vijana wa Sisi Tambala waliokuwapo kati...
No comments:
Post a Comment