Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limemthibitisha Mizengo Kayanza Peter Pinda kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania kuchukua nafasi ya Edward Lowassa aliyejizulu jana.
Mizengo Pinda anakuwa Waziri Mkuu wa 10 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akitanguliwa na JK Nyerere, Rashid Kawawa, Cleopa Msuya, Edward Sokoine, Salim Ahmed Salim, Joseph Warioba, John Malecela, Fredrick Sumaye na Edward Lowassa.
Akitangaza matokeo sasa hivi Spika wa Bunge Samwel Sitta, Pinda amepitishwa rasmi na wabunge kuwa Waziri Mkuu mpya kwa kura 279 za ndio ama asilimia 98.9 wakati kura mbili za hapana na moja imeharibika.
Kuanzia dakika hii mheshimiwa Mizengo Peter Pinda ndiye Waziri Mkuu wetu. Saa tano kamili kesho ataapishwa Ikulu ya Chamwino.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
RAIS SAMlA AFANYA MAZUNGUMZO NA MJUMBE MAALUM WA RAIS TSHISEKEDI
Dar es Salaam, 26 Machi 2025 – Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan , amekutana na kufanya mazungu...
-
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu na timu ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa akiwa katika ...
-
(Picha na Yahya Charahani) Kwa wale waliokulia maeneo haya, hili ni jambo la kawaida ukitoka mjini, shambani sijui hadi wapi kote ni haya h...
-
NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA PSLE-2014 EXAMINATION RESULTS ARUSHA DAR ES SALAAM DODOMA IRINGA KAGERA KIGOMA ...
No comments:
Post a Comment