Tuesday, July 15, 2014

WAZIRI LAZARO NYALANDU AKUTANA NA TAASISI ZA MBALIMBALI ZINAZOJIHUSISHA NA UHIFADHI WANYAMAPORI JIJINI NEW YORK – MAREKANI,

1   
Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi Waandamizi wa Taasisi ya Vulcan ya nchini Marekani Bw. Dave Stewart (kushoto) na Bi. Lauren Ryder, inayojihusisha na masuala ya kuidadi tembo katika nchi 18 barani Afrika ikiwemo Tanzania, baada ya kufanya mazungumzo maalum ya ushirikiano yaliyofanyika katika jiji la New York nchini Marekani jana.
2
Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu akiagana na Bw. Dave Stewart kutoka Taasisi ya Vulcan inayojihusisha na masuala ya kuidadi tembo katika nchi 18 barani Afrika ikiwemo Tanzania mara baada ya kumaliza mazungumzo nao jana jijini New York nchini Marekani.
4
Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu akizungumza na Balozi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa Balozi Tuvako Manongi mara baada ya kukamilika kwa kikao jana baina ya Waziri Nyalandu na ujumbe wake pamoja na taasisi mbalimbali za uhifadhi jijini New York, Marekani. Kati ni Katibu wa Waziri Bw. Imani Nkuwi.
3
Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu (watatu kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi Waandamizi wa Taasisi ya inaundwa na Wanajeshi Wastaafu wa jeshi la Marekani walioanzisha umoja wao ujulikanao kama (VETPAW)kwa ajili ya kusaidia Uhifadhi wa Wanyamapori barani Afrika mara baada ya kumaliza mazungumzo baina yao jana jijini New York, Marekani. Kushoto ni Balozi wa Kudumu wa Tanzania Umoja wa Mataifa Balozi Tuvako Manongi.

No comments: