Tuesday, July 15, 2014

Waziri Dk. Mwakyembe azungumzia Taarifa ya Mkutano Baina ya Mawaziri wa Uchukuzi na Fedha Kutoka Tanzania na Zambia Uliofanyika hivi Karibuni Jijini Lusaka nchini Zambia


Waziri wa Uchukuzi Dkt. Harrison Mwakyembe  akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) mapema hii leo Jijini Dar es Salaam wakati alipokuwa akizungumzia mikakati ya Wizara yake katika kutatua changamoto zinazolikabiri Shirika la Reli laTanzania na Zambia (TAZARA).

Waandishi wahabari wakimfuatilia kwa makini Waziri wa Uchukuzi Dkt. Harrison Mwakyembe  (hayupo pichani) mapema hii jana Jijini Dar es Salaam wakati alipokuwa akizungumzia mikakati ya Wizara yake katika kutatua changamoto zinazolikabiri Shirika la Reli laTanzania na Zambia (TAZARA). Picha zote na Eliphace Marwa
--
Na Rose Masaka, SJMC

Sheria ya uanzishwaji na uendeshaji wa Shirika la Reli TAZARA kuboreshwa ili kutoa fursa kwa Shirika hilo kujiendesha Kibiashara.

Haya yamebainishwa na Waziri wa Uchukuzi wa Tanzania Dkt. Harrison Mwakyembe alipokutana na wandishi wa Habari leo jijini Dar es Salaam ili kutoa taarifa ya mkutano baina ya Mawaziri wa Uchukuzi na Fedha kutoka Tanzania na Zambia uliofanyika hivi karibuni jijini Lusaka nchini Zambia

Dkt. Mwakyembe alisema kuwa mpaka sasa Tanzania imekwisha wasilisha mapendekezo ya maboresho ya Sheria hiyo na kuongeza kuwa kinachosubiriwa ni ni kwa upansde wa Zambia kukamilisha taribu ambapo watawasilisha marekebisho hayo mwezi ujao.

Aidha Mwakyembe aliongeza kuwa pamoja na marekebisho hayo ya Sheria washirika wa TAZARA wamefikia maamuzi ya kuondoa madaraka ya Shirika hilo kutoka Makao Makuu na kuyapeleka katika ngazi ya Mikoa ambayo ni Tanzania na Zambia,

Kufuatia muundo huo mpya kila mkoa utashughulika na masuala yote ya ndani kama kusimamia Treni za abiria na uchukuzi wa mizigo ya ndani ya nchi wakati Makao makuu yatashughulika na masuala yanayovuka mipaka baina ya nchi hizo mbili.

‘Tanzania itaanza na safari za majaribio kwa muda wa miezi mitatu huku ikifanya safirisha abiria na mizigo mara mbili kwa wiki ambazo ni siku ya jumanne na ijumaa” Alisema Mwakyembe.

Wakati huo huo Waziri Mwakyembe ameongeza kuwa Serikali imekusudia kuanzishwa safari ya Treni maalum kutoka Makambako kupitia Mlimba – Msolwa hadi Mkamba ili kuondoa adha ya usafiri kwa wakazi wa maeneo hayo.

Dkt.Mwakyembe amesema kuwa Treni hiyo Maalum yenye mabehewa matano ya abiria na behewa la mizigo itasaidia katika mnaeneo hayo kwakuwa ni jiografia yake ni ya miinuko. 

Mkutano wa Mawaziri hao ulifanyika ikiwa ni desturi ya viongozi wa nchi washirika wa TAZARA, Tanzania inatarajiwa kuwa mwenyeji wa Mkutano  huo mapema mwezi Agosti .

No comments: