Tuesday, July 08, 2014

BALOZI WA TANZANIA NCHINI UBELIGIJI, MH. KAMALA ATEMBELEA BANDA LA MFUKO WA PENSHENI WA PPF KATIKA MAONYESHO YA SABASABA‏


Meneja Uhusiano na Masoko wa Mfuko wa Pensheni, Lulu Mengele (kushoto) akimkaribisha Balozi wa Tanzania Nchini Ubelgiji, Mh Dodorius Kamala (kulia) wakati alipotembelea banda la PPF kwenye maonyesho ya Sabasaba yanayomalizika hivi leo.
 Afisa Mafao wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Hellen Mollel akitoa maelezo kwa Balozi wa Tanzania Nchini Ubeligiji, Mh Kamala juu ya wanachama wanavyonufaika na mafao wakati wanapostaafu kazini, Wa kwanza Kushoto ni Meneja Uhusiano na Masoko, Lulu Mengele


Afisa Uwekezaji wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Anna Shayo akimpa maelekezo Balozi wa Tanzania Nchini Ubeligiji, Mh Kamala namna PPF wanavyotumia michango ya Wanachama wao katika kuwekeza katika miradi mbalimbali ambayo baadhi ya miradi hiyo tayari ishaanza kufanya kazi.


Balozi wa Tanzania Nchini Ubeligiji, Mh D.Kamala akiagana na Meneja Uhusiano na Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Lulu Mengele mara baad`a ya kumaliza kutembelea banda la PPF kwenye maonyesho ya Sabasaba yanayomalizika hivi leo.Picha zote na Josephat Lukaza - Lukaza Blog

No comments:

WIZARA YA AFYA YAOMBA SH. TRILIONI 1.8 BAJETI YA 2026/2027

  Wizara ya Afya imeomba kuidhinishiwa jumla ya Shilingi trilioni 1.8 kwa mwaka wa fedha 2026/2027 kwa ajili ya kuendelea kuboresha huduma z...