Thursday, July 03, 2014

TWIGA BANCORP YAENDELEA KUTOA HUDUMA ZAKE NDANI YA VIWANJA VYA SABA SABA JIJINI DAR

 Katika kuboresha huduma za kibenki Twiga Bancorp,Afisa wa Benki hiyo,pichani kati Bi Tuddy Lutengano akimhudumia mteja pichani kulia katika banda lao lililopo kwenye maonyesho ya 38 ya Biashara ya Kimataifa yanayofanyika katika viwanja vya Mwl.Julius Nyerere, KuShoto ni Meneja wa Tawi lililopo ndani ya Maonyesho hayo,Bi. Upendo Tendewa akihakikisha huduma bora za kibenki zinafanyika na kukidhi haja kwa  wateja wao.
 Muonekano banda la Benki ya Twiga Bancorp lionekanavyo kwa nje ndani ya maonyesho ya 38 ya Biashara ya Kimataifa yanayofanyika katika viwanja vya Mwl.Julius Nyerere,jijiniDar.
 Baadhi ya Wateja wakipata huduma za kibenki ndani ya Twiga Bancorp 
 Mmoja wa wateja wa Twiga Bancorp akipata maelezo kwa ufupi kuhusiana na huduma mbalimbali zitolewazo na benki hiyo.
 Karibu:Baadhi ya Wafanyakazi wa Twiga Bancorp wakiwa nje ya banda lao kwenye maonyesho ya 38 ya Biashara ya Kimataifa yanayofanyika katika viwanja vya Mwl.Julius Nyerere,jijini Dar.

No comments:

TANZANIA INA FURSA KUBWA YA KUENDELEZA NISHATI YA JOTOARDHI; WAZIRI NDEJEMBI ALIELEZA BARAZA LA IRENA

📌Asisitiza ushirikiano wa taasisi za kifedha na Jumuiya za Kimataifa hasa katika hatua za utafiti 📌Akaribisha wawekezaji; Asema Serikali i...