Wednesday, August 10, 2016

MAKAME MBARAWA AZINDUA TRENI YA PILI DAR


Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa amezindua treni ya pili ya abiria jijini Dar es Salaam, inayofanya safari zake kuanzia kituo kikuu cha stesheni hadi Pugu.

Akizungumza mara baada ya kuzindua treni hiyo Waziri Mbarawa amesema kuwa serikali imejipanga usafiri huo kuwa endelevu ili kupunguza msongamano wa magari katika jiji la Dar es Salaam.
Waziri Mbarawa amesema treni hiyo yenye uwezo wa kubeba abiria 1500 kwa wakati mmoja itasaidia kwa kiasi kikubwa kuondoa msongamano na kuwahisha shughuli za maendeleo kwa wakazi wa jiji la Dar es Salaam.
Aidha waziri Mbarawa amesema kuwa takribani magari 46 yanayobeba abiria 35 yatakuwa yamepungua kutokana na treni hiyo ambayo licha ya changamoto zilizokuwepo ameahidi kushughulikia ili usafari huo uweze kudumu kwa muda mrefu.

No comments:

MAKAMU WA PILI WA RAIS ZANZIBAR AMTEMBELEA MHE. FARIDA AMOUR MOH'D HOSPITALINI, AMTAKIA AFYA NJEMA

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla , leo tarehe 21 Mei 2026 amemtembelea na kumjulia hali Mwakilishi wa Viti M...