Wednesday, August 10, 2016

MAKAME MBARAWA AZINDUA TRENI YA PILI DAR


Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa amezindua treni ya pili ya abiria jijini Dar es Salaam, inayofanya safari zake kuanzia kituo kikuu cha stesheni hadi Pugu.

Akizungumza mara baada ya kuzindua treni hiyo Waziri Mbarawa amesema kuwa serikali imejipanga usafiri huo kuwa endelevu ili kupunguza msongamano wa magari katika jiji la Dar es Salaam.
Waziri Mbarawa amesema treni hiyo yenye uwezo wa kubeba abiria 1500 kwa wakati mmoja itasaidia kwa kiasi kikubwa kuondoa msongamano na kuwahisha shughuli za maendeleo kwa wakazi wa jiji la Dar es Salaam.
Aidha waziri Mbarawa amesema kuwa takribani magari 46 yanayobeba abiria 35 yatakuwa yamepungua kutokana na treni hiyo ambayo licha ya changamoto zilizokuwepo ameahidi kushughulikia ili usafari huo uweze kudumu kwa muda mrefu.

No comments:

SAMIA AZINDUA MKUTANO WA KIMATAIFA WA WFNS, ATEMBELEA MAONESHO YA SEKTA YA AFYA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akitembelea mabanda ya maonesho ya wadau wa Sekta ya Afya kabla ya k...