Wednesday, August 17, 2016

ALIYEKUWA MKURUGENZI WA VITAMBULISHO VYA TAIFA (NIDA) NA WENZAKE NANE WAFIKISHWA MAHAKAMANI


 
Mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya vitambulisho vya taifa-NIDA- Dickson Maimu (wa tatu kushoto) na viongozi wengine  nane wa taasisi hiyo wamefikishwa katika mahakama ya hakimu mkazi kisutu mapema leo.Habari zaidi tutawaletea.

Mnamo mwezi January 2016, Rais Magufuli aliamua kutengua uteuzi wa Mkurugenzi wa mamlaka ya vitambulisho vya taifa (NIDA) Bwana Dickson Maimu na kumsimamisha kazi yeye na wafanyakazi wengine ili kupisha uchunguzi wa namna ilivyotumika kiasi cha shilingi bilioni 179.6 katika zoezi la upatikanaji wa vitambulisho vya taifa wakati bado kuna malalamiko kwamba watu wengi hawajapata vitambulisho hivyo. .

No comments:

BILIONI 37.7 ZATIKISA TANGA: TARURA YASUKUMA MAPINDUZI YA BARABARA

MAMLAKA ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) mkoa wa Tanga imepiga hatua kubwa katika utekelezaji wa miradi ya miundombinu ya baraba...