Taarifa zilizotufikia hivi karibuni zinasema kuwa mzee wa vijisenti na Waziri wa zamani wa Miundombinu bwana John Chenge amepandishwa kizimbani katika mahakama ya hakimu mkazi kinondoni na kusomewa mashitaka matatu ya kusababisha vifo vya watu watatu.
Alitinga mahakamani hapo akiwa ametilia viwalo vyake kama kawaida huku akitoa tabasamu kama ilivyo kawaida yake huku akisubiriwa na watu kibao, huku wengine wakionekana kuwa na shauku ya kutaka kumwona 'live' na wengine wakipiga vikelele kelele vidogo wakisema muzee wa vijisenti.
Yeye mwenye alionekana kuwa kawaida tu. Aliwasili na gari jingine VX na akaondoka na gari jingine. Kwa jinsi watu walivyokuwa kibaoi ilibidi apitie mlango wa nyuma na tena wa mahakama ya mwanzo ya kinondoni na kupuruchuka zake tim. Amejidhamini mwenye kwa kiasi cha Sh milioni moja. Kesi itatajwa tena siku itakayotajwa baadaye.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
RAIS SAMIA ASHIRIKI NA KUTUNUKU TUZO ZA WASANII WA KOMEDI TANZANIA 2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameshiriki kama mgeni rasmi katika hafla ya utoaji wa Tuzo za Wasa...

-
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu na timu ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa akiwa katika ...
-
(Picha na Yahya Charahani) Kwa wale waliokulia maeneo haya, hili ni jambo la kawaida ukitoka mjini, shambani sijui hadi wapi kote ni haya h...
-
NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA PSLE-2014 EXAMINATION RESULTS ARUSHA DAR ES SALAAM DODOMA IRINGA KAGERA KIGOMA ...
No comments:
Post a Comment