Taarifa zilizotufikia hivi karibuni zinasema kuwa mzee wa vijisenti na Waziri wa zamani wa Miundombinu bwana John Chenge amepandishwa kizimbani katika mahakama ya hakimu mkazi kinondoni na kusomewa mashitaka matatu ya kusababisha vifo vya watu watatu.
Alitinga mahakamani hapo akiwa ametilia viwalo vyake kama kawaida huku akitoa tabasamu kama ilivyo kawaida yake huku akisubiriwa na watu kibao, huku wengine wakionekana kuwa na shauku ya kutaka kumwona 'live' na wengine wakipiga vikelele kelele vidogo wakisema muzee wa vijisenti.
Yeye mwenye alionekana kuwa kawaida tu. Aliwasili na gari jingine VX na akaondoka na gari jingine. Kwa jinsi watu walivyokuwa kibaoi ilibidi apitie mlango wa nyuma na tena wa mahakama ya mwanzo ya kinondoni na kupuruchuka zake tim. Amejidhamini mwenye kwa kiasi cha Sh milioni moja. Kesi itatajwa tena siku itakayotajwa baadaye.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Prof. Mfaransa Aja na Kitabu: Aiambia Dunia Kutalii Tanzania ni Tiba
Na Mwandishi Wetu Paris, Ufaransa Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana, akiwa nchini Ufaransa jana Julai 8, 2025 amek...

-
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu na timu ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa akiwa katika ...
-
NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA PSLE-2014 EXAMINATION RESULTS ARUSHA DAR ES SALAAM DODOMA IRINGA KAGERA KIGOMA ...
-
Mwanamuziki toka Jamhuri ya KIdemokrasia ya Kongo, Mbilia Bel akitumbuiza katika viwanja vya bunge mjini Dodoma jana. Picha na Jube Tranquil...
No comments:
Post a Comment