Thursday, March 19, 2009

Rais Kikwete arejea nchini


Rais Jakaya Mrisho Kikwete amerejea nyumbani leo, Alhamisi, Machi 19, 2009, akitokea London, Uingereza, ambako mwanzoni mwa wiki hii alihudhuria mkutano maalum wa maandalizi ya Mkutano wa Nchi za G-20, kuzungumzia matatizo makubwa yanayoukabili uchumi wa dunia.

Kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar Es salaam, Rais Kikwete amelakiwa na viongozi mbali mbali wa Serikali wakiongozwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

Rais Kikwete alikuwa miongoni mwa viongozi wanane wa Bara la Afrika walioalikwa na Waziri Mkuu wa Uingereza Gordon Brown kuwakilisha msimamo wa Afrika kama nchi za Afrika zinavyoutaka uelezwe kwenye Mkutano wa G-20, uliopangwa kufanyika mwanzoni mwa mwezi ujao hapo hapo London.

Viongozi wengine wa Afrika waliohudhuria mkutano huo wa maandalizi uliofanyika Jumatatu, Machi 16, 2009, kwenye Jumba la Lancaster House chini ya uenyekiti wa Gordon Brown ni pamoja na Rais Khama Ian Khama wa Botswana, na Rais Ellen Johnson Sirleaf.

Wengine ni Waziri Mkuu wa Ethiopia Meles Zenawi, Waziri Mkuu wa Kenya Raila Odinga, Waziri wa Fedha wa Afrika Kusini Trevor Manuel, Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika (AU) Jean Ping, na Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Donald Kaberuka.

Viongozi hao kwa pamoja walimweleza Gordon Brown msimamo wa Afrika ambao wanataka uwasilishwe katika Mkutano huo wa G-20 ikiwa ni pamoja na:

No comments: