Wednesday, March 11, 2009

Usaili wa shindano la Bongo Star Search uliofanyika mjini Kigoma mwishoni mwa wiki hii umevunja rekodi ya usaili wote ulofanyika huko nyuma kwa mwaka huu.

Washiriki wa usaili huo kutoka Kigoma Vijijini, Ujiji, Mwanga, Mwandiga, Katonga, Kibirizi, Ilagala, Bitare, Karago, Simbo, Kidahwe, Kalenge na Kazura mimba, familia zao na marafiki walijazana katika ukumbi maarufu wa Chama cha Msalaba Mwekundu.

Ingawa umati ulohudhuria ulikuwa mkubwa, lakini majaji hawakuweza kupata kipaji chochote ambacho kingewea kuwakilisha mkoa wa Kigoma na wakaamua kuchagua wawili ili wawakilishe mkoa huo. Habari hii ya Henry Mdimu.

1 comment:

Anonymous said...

hao majaji yawezekana waliweka negative attitude kwa mkoa na washiriki, lakini wakumbuke kwa miaka yote miwili ya uhai wa shindano lao mkoa huo umekuwa unatoa vipaji vingi, hata kwa waliochaguliwa kutokea mikoa mingine wenye asili ya mkoa huo.pia katika bongo flava mkoa huo ni wa pili ukitoka mbeya kwa kuwa na jijana wengi aktika fani.
poa tu, hao hao wawili watafika mbali.