Wednesday, March 18, 2009

Mambo ya maisha plus











Mdau Pius katubandikia taarifa muhimu za vijana wetu wa Maisha Plus akisema kuwa Washiriki wawili waliokuwa wakiwakilisha kanda ya kati, Efrancia Mangii (kulia) na Peter Putir (Shoto) wameliaga shindano la Maisha Plus hilo huku Maulid Wadi akirejea baada ya kupata kura nyingi.
Washiriki hao wamefungua dimba la kuaga katika shindano hilo lililoanza wiki mbili zilizopita. Shindano hilo linabakiwa na mshiriki mmoja anayewakilisha kanda hiyo, Juma Madaraka.
Wakati huohuo Putir ameapta shavu la kutangaza katika kituo cha redio cha TBC Fm mara baada ya utolewa katia shindano hilo.
Mkurugenzi wa TBC, Tido Mhando aliitangaza ofa hiyo wa Putir baada ya uvutiwa na sauti nzuri ya mshiriki huyo.

1 comment:

ghalib shariff said...

mimi ni mtazamaji wa kipindi cha maisha plus kuanzia washiriki wanachaguliwa maoni yangu ni maulidi wadi ni kijana ambae anajaribu sana kuishi maisha ya kijijini lakini la msingi ambalo ni ngependa kusema kwa nini hakukuwa na upimaji wa H.I.V wakati wakiwa pamoja huwenda wengine labda wameathirika na hatujui?na wote ni vijana damu zao ziko moto ...ghalib shariff kutoka mtwapa mombasa kenya