Monday, May 31, 2010

Mchakato wa kumfanya Mwalimu Nyerere kuwa Mtakatifu


Rais Museveni akimkaribisha Mama Maria Nyerere shereheni huko Namugogo wikiendi hii. Chini akimwagilia mti alioupanda kama kumbukumbu ya siku hii
Hizi ni baadhi ya picha za mchakato wa kumuombea baba wa taifa Mwalimu Julius Nyerere kuwa mwenyeheri na baadaye kuwa Mtakatifu. Huwezi kuwa mtakatifu kabla hujawa mwenyeheri.
Kesho kutakuwa na ibada ya kumuombea Mwalimu Nyerere kuwa Mwenyeheri na hatimaye kuwa Mtakatifu katika kanisa lilipo Namugongo ambapo inatarajiwa kuwa marais au wawakilishi kutoka katika baadhi ya nchi za Afrika watahudhuria ibada hiyo.
Familia ya Mwalimu iliwasili Hapa uganda Jumamosi kwa ajili ya Ibada hiyo. Mbali na familia ya baba wa taifa mamia kwa maelfu ya watanzania pia wameondoka nchini 28 kuelekea huko namugongo kwa ajili ya ibada ya hija inayofanyika kila mwaka June 3 katika kanisa hilo.
Mama Maria yuko pamoja na Kikundi cha sala za wanamaombi cha Marian Healing faith Centre cha River Side, Ubungo jijini Dar. PICHA NA HABARI KWA HISANI YA Michuzi

No comments: