Monday, May 03, 2010

Barabara kufungwa kwa saa tatu



Leo Mkuu wa Mkoa wa DSM William Lukuvi, ametangaza rasmi kufungwa kwa
barabara 3 muhimu kwa masaa machache mpaka mkutano wa World Economic Forum
uishe. barabara hizo ni Sam Nujoma, Nyerere na Bagamoyo Rd (Ali Mwinyi Rd)

Kufungwa barabara ya Bagamoyo ni kuhamishia watumiaji barabara hiyo Old
Bagamoyo road, sasa hivi tu kwa wale watumiaji wanakoma ubishi kwasababu
foleni ni masaa yote sasa hivi kutokana na miundo mbinu mibovu, sasa
wakiamishia watumiaji wengine wote si itakuwa balaa.

Anasema Mkuu wa mkoa kwamba ni kuanzia saa moja asubuhi mpaka saa 3 na
kufngwa tena jioni saa tisa mpaka saa kumi na mbili jioni, sasa mimi
navyojua hii ndio pick hrs yenyewe, sasa si uchumi wote utasimama.

No comments: