Monday, May 03, 2010

Watoto waliouawa wazikwa



MIILI ya watoto watatu waliouawa na mama yao mzazi kwa kukatwakatwa na shoka Alhamisi iliyopita imezikwa leo nyumbani kwao eneo la Kariwa kata ya Longuo B manispaa ya Moshi Mkoani Kilimanjaro.

Taarifa iliyotolewa na baba mzazi wa watoto hao, Aloyce Thadei alisema kuwa ibada ya mazishi ya kuaga watoto hao itafanyika katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) dayosisi ya kaskazini usharika wa KCMC.

Thadei alisema watu mbalimbali wakiwemo viongozi wa serikali wanatarajiwa kuhudhuria msiba huo ambao ni wakuhuzunisha na kuwa tayari ndugu wa karibu waliokuwa wanasubiriwa tayari wameshafika.

Watoto waliouawa na mama yao ni Rose Thadei (12) ambaye ni mlemavu wa akili na viungo, Noel Thadei (5) na Antony Thadei (2).

No comments:

Dkt. Samia: Tumeweka fedha nyingi katika Umwagiliaji kukabili Mabadiliko ya Tabianchi

Rais Dkt .Samia Suluhu Hassan, amesema katika kufikia azma ya mapinduzi sekta ya kilimo Serikali imechukua hatua ya kufanya uwekezaji mkubwa...