Sunday, May 23, 2010

Jamal Khan wa Dar aibuka mshindi mbio za Magari Zig Zag

Pichani Ally Kiraka wa Tanga na Ahmed Aslam wakifurahi baada ya kukabidhiwa kombe la ushindi wa sita.

Mshindi wa mbio za magari Tanga Rally Zig Zag 2010 Jamil Khan na msoma ramani wake Rahim Suleyman
wakifurahia baada ya kupokea kikombe cha ushindi katika viwanja vya Popatlal Jijini Tanga,alitumia gari aina ya Subaru Imreza na kukimbia kwa muda wa saa 1.33.44.

Dereva mkongwe katika mashindano ya
mbio za magari Afrika Mashariki,Jayant Shah (70) akipokea kombe la ushindi wa tatu katika mashindano ya Tanga Rally 2010 na Mkuu wa Wilaya ya Tanga,Ibrahimu Msengi,mkongwe huyo alishiriki kwa kuendesha gari aina ya Dutsun 260z iliyotengenezwa mwaka 1975 akiwa na msoma ramani wake Radhi Chana waliotumia saa 1.43.53.

No comments:

PROF. SHEMDOE AWAASA WANAFUNZI KUENDELEZA VIPAJI VYAO VYA MICHEZO, SANAA

• Awataka kuwa na nidhamu na kusoma kwa bidii Na OWM - TAMISEMI, Iringa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali ...