Friday, May 16, 2014

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,Bernard Membe Afungua Rasmi Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara Ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Jijini Dar es Salaam

 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.)-katikati) kwa pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John Haule (wa tatu kutoka kushoto) na viongozi wengine wakiimba wimbo wa "Solidarity" wakati wa ufunguzi wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa uliofanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam tarehe 15 Mei, 2014.
 Katibu Mkuu, Bw. Haule nae akizungumza wakati wa ufunguzi wa Baraza hilo.
 Mkurugenzi wa Idara ya Afrika na Mjumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Baloiz Vincent Kibwana akitoa neno la shukrani kwa niaba ya Wajumbe wa Baraza hilo.
 Katibu wa Baraza la Wafanyakazi, Bibi Naomi Zegezege nae akizungumza wakati wa ufunguzi wa Baraza hilo huku Mhe. Membe na Viongozi wengine wakimsikiliza.
 Mhe. Membe akitoa hotuba ya ufunguzi wa Baraza la Wafanayakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ambapo alitoa rai kwa Wafanyakazi hao kujituma na kuongeza bidii katika utendaji kazi wao wa kila siku.
 Katibu Mkuu, Bw. Haule, Naibu Katibu Mkuu, Balozi Rajabu Gamaha na Viongozi wengine wakifurahia jambo wakati wa kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Mambo ya Nje.

No comments: