Tuesday, May 06, 2014

JAJI BOMANI‏: ANDIKENI HABARI ZA KUMKOMBOA MWANANCHI

 Mshehereshaji ambaye ni Mwanakamati ya maandilizi ya maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani 2014, Usia Nkhoma Ledama akiwatambulisha baadhi ya waandishi wa habari wakongwe (hawapo pichani) kwa mgeni rasmi Jaji Mstaafu Mark Bomani.(Picha zote na Zainul Mzige).
DSC_0171
Baadhi ya waandishi wa habari wakongwe (Ma-veterans) wakimsalimia mgeni rasmi.…
Mshehereshaji ambaye ni Mwanakamati ya maandilizi ya maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani 2014, Usia Nkhoma Ledama akiwatambulisha baadhi ya waandishi wa habari wakongwe (hawapo pichani) kwa mgeni rasmi Jaji Mstaafu Mark Bomani.(Picha zote na Zainul Mzige).
DSC_0171
Baadhi ya waandishi wa habari wakongwe (Ma-veterans) wakimsalimia mgeni rasmi.
DSC_0077
Meza Kuu, kutoka kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Elimu, Sayansi na Mawasiliano ya Umoja wa Mataifa (UNESCO) Bw. Abdul Wahab Coulibaly, Mkurugenzi wa Mfuko wa Vyombo vya Habari Tanzania (TMF) Bw. Ernest Sungura, Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Bw. John Mongela, Mgeni rasmi Jaji Mstaafu Mark Bomani, Mwenyekiti wa Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika, Tawi la Tanzania (MISA-TAN), Bw. Mohamed Tibanyendera, Rais wa Umoja wa Vilabu vya Waandishi wa habari Tanzania (UTPC) Bw. Kenneth Simbaya na Meneja Utafiti na Ushapishaji wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), Bw. John Mirenyi.
DSC_0348
Mgeni rasmi Jaji Mstaafu Mark Bomani, akitoa risala wakati wa maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani 2014 yaliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa AICC jijini Arusha mwishoni mwa juma.
DSC_0429
Sehemu ya wadau wa tasnia ya Habari wakisikiliza risala ya mgeni rasmi.
DSC_0329
Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Bw. John Mongela akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa wa Arusha kwenye maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika jijini Arusha kenye ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa AICC.
DSC_0112
Mwenyekiti wa Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika, Tawi la Tanzania (MISA-TAN), Bw. Mohamed Tibanyendera, akizungumza kwenye maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani 2014 yaliyofanyika kwenye ukumbi wamikutano wa Kimataifa wa AICC jijini Arusha.
DSC_0163
Wageni waalikwa na wadau wa tasnia ya habari wakiwa kwenye ukimya kumkumbuka Mwandishi aliyeuwawa mkoani Iringa Daudi Mwangosi.
DSC_0188
Mkurugenzi wa Shirika la Elimu, Sayansi na Mawasiliano ya Umoja wa Mataifa (UNESCO) Bw. Abdul Wahab Coulibaly, akitoa Ujumbe wa Pamoja wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa na Mkurugenzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Irina Bokovas kuhusiana na Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani 2014.
DSC_0217
Meneja Machapisho, Utafiti na Uhifadhi Hati wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), Bw. John Mirenyi, akitoa maelezo ya machapisho mbalimbali yaliyoandaliwa na baraza hilo yakiwemo yenye madhila mbalimbali yaliwahi kuwakumba baadhi ya waandishi wa habari ndani na nje ya nchi.
DSC_0241
Mkurugenzi wa Mfuko wa Vyombo vya Habari Tanzania (TMF) Bw. Ernest Sungura, akizungumzia mchango wa mfuko huo unaowawezesha waandishi wa habari kutafuta habari za uchunguzi na zinazoigusa jamii.
DSC_0247
Wasanii wa Bendi ya Mrisho Mpoto (Mjomba Band) wakitoa burudani kwa wageni waalikwa wakati wa maadhimisho ya siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani 2014 yaliyofanyika jijini Arusha mwishoni mwa juma.
DSC_0156
Sehemu ya wadau wa tasnia ya habari wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri ukumbini hapo.
DSC_0259
Katibu wa Chama cha Wamiliki wa Vyombo vya Habari nchini (MOAT), Henry Muhanika, akisoma hotuba kwa niaba ya Dr. Reginald Mengi kwenye maadhisho hayo.
DSC_0269
Rais wa Umoja wa Vilabu vya Waandishi wa habari Tanzania (UTPC) Bw. Kenneth Simbaya, akizungumzia wakati wa maadhimisho hayo.
DSC_0286
Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri (TEF), Absalom Kibanda, akizungumzia changamoto mbalimbali zinazowakumba waandishi wa habari wakati maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani 2014 yaliyofanyika jijini Arusha.
DSC_0288
Mkurugenzi wa TAMWA, Bi. Valerie Msoka, akizungumzia changamoto za usawa wa Kijinsia katika uongozi kwenye Vyombo vya Habari nchini.
DSC_0304
Meneja Uhusiano wa TANAPA, Pascal Shelutete, akizungumzia ushiriki wao kwenye Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani 2014 ambapo aliwataka waandishi wahabari kutumia kalamu zao vizuri katika kukuza Utalii wa Tanzania ndani na nje ya nchi.

No comments: