Monday, May 12, 2014

BENKI YA EXIM YAISAIDIA WODI YA WAZAZI YA HOSPITALI YA RUFAA YA MWANANYAMALA

MWN PIX 1Meneja Msaidizi Masoko wa Benki ya Exim Tanzania, Bi Anita Goshashy (Watatu Kushoto) akikabidhi magodoro kwa Mganga Mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya Mwananyamala, Dkt. Sophinias Ngonyani (Kushoto). Wakishuhudia ni Wafanyakazi wa Benki ya Exim.  Benki ya Exim imetoa magodoro 60 katika Wadi ya Wazazi katika Hospitali ya Rufaa ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki katika kuadhimisha Siku ya Mama Duniani. Picha na Mpiga Picha Wetu. MWN PIX 4MWN PIX 5Meneja Msaidizi Masoko wa Benki ya Exim Tanzania, Bi Anita Goshashy (Watatu Kushoto) akikabidhi magodoro kwa Mganga Mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya Mwananyamala, Dkt. Sophinias Ngonyani (Kushoto). Wakishuhudia ni Wafanyakazi wa Benki ya Exim.  Benki ya Exim imetoa magodoro 60 katika Wadi ya Wazazi katika Hospitali ya Rufaa ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki katika kuadhimisha Siku ya Mama Duniani. Wa kwanza kushoto ni Muuguzi Kiongozi Sr. Tuswege Mwamwaja na Kulia ni Muuguzi Mkunga Bi. Marietha Mwageni. (Picha na Mpiga Picha Wetu)MWN PIX 6Meneja Msaidizi Masoko wa Benki ya Exim Tanzania, Bi Anita Goshashy (Wakwanza Kushoto)  na Meneja Msaidizi Msoko mwenzake Bi Violet Bikoche (Wapili Kushoto) wakizungumza na mmoja kati ya kinamama waliojifungua mara baada ya kukabidhi magodoro katika Hospitali ya Rufaa ya Mwananyamala.  Benki ya Exim imetoa magodoro 60 katika Wodi ya Wazazi Hospitalini hapo mwishoni mwa wiki katika kuadhimisha Siku ya Mama Duniani. (Picha na Mpiga Picha Wetu).MWN PIX 7Muuguzi Kiongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Mwananyamala Sr. Tuswege Mwamwaja (wa kwanza kulia) akifafanua jambo kwa wafanyakazi wa Benki ya Exim Tanzania mara baada ya Benki hiyo kukabidhi magodoro 60 katika Wodi ya Wazazi Hospitalini hapo mwishoni mwa wiki katika kuadhimisha Siku ya Mama Duniani. (Picha na Mpiga Picha Wetu). MWN PIX 8Katibu wa Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Exim Bi. Erica Mbutu (wakwanza kushoto) na Meneja Msaidizi Msoko wa Benki ya Exim, Bi Violet Bikoche (Wapili Kushoto) wakizungumza na mmoja kati ya kinamama waliojifungua mara baada ya kukabidhi magodoro katika Hospitali ya Rufaa ya Mwananyamala.  Benki ya Exim imetoa magodoro 60 katika Wodi ya Wazazi Hospitalini hapo mwishoni mwa wiki katika kuadhimisha Siku ya Mama Duniani. (Picha na Mpiga Picha Wetu).MWN PIX 9Mganga Mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya Mwananyamala Dkt. Sophinias Ngonyani (wa kwanza kulia) akifafanua jambo kwa wafanyakazi wa Benki ya Exim Tanzania mara baada ya Benki hiyo kukabidhi magodoro 60 katika Wodi ya Wazazi Hospitalini hapo mwishoni mwa wiki katika kuadhimisha Siku ya Mama Duniani. (Picha na Mpiga Picha Wetu).
Na Mwandishi Wetu
BENKI ya Exim ya Tanzania imeadhimisha Sikukuu ya Mama Duniani kwa kuchangia magodoro 60 katika wodi ya wazazi ya Hospitali ya Mwananyamala iliyopo jijini Dar es Salaam katika kutoa heshima kwa kinamama wote na kuunga mkono jitihada za kuboresha afya ya uzazi nchini. 
Kwa sasa, Hospitali ya Mwananyamala ambayo ni hospitali kubwa ya rufaa jijini Dar es Salaam inatoa huduma kwa wakinamama wanaotarajia kujifungua zaidi ya 3100 kwa mwezi, ikiwa na vitanda 136 tu katika wodi hiyo ya wazazi.
Akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi magodoro hayo hospitali hapo jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki, Meneja Msaidizi Masoko Bi Anita Goshashy alisema mchango huo ni moja kati ya utekelezaji wa shughuli za benki yake zinazolenga kuisaidia jamii inayoizunguka.
 “Mwaka jana, Benki ya Exim imeweza kufikia faida ya shilingi bilioni 20, na tumekuwa na utamaduni wa kurejesha kile tukipatacho toka kwa jamii. Sasa, leo hii tuko hapa Mwananyamala kukabidhi vitu hivi, ikiwa kama njia ya kutambua mchango wa kina mama zetu na kuonyesha jinsi gani tunaisaidia jamii inayotuzunguka kama benki,” alisema Bi. Goshashy, aliongeza kuwa benki itaendelea kuipiga jeki jamii hususani katika sekta ya Afya, Mazingira na Elimu.
Bi. Goshashy alisisitiza kuwa, “Leo hii tunakabidhi magodoro haya ili kuweza kusaidia kuboresha uzazi uliosalama. Kina mama wengi wanaotarajia kujigfungua ufariki wakati wakijifungua. Mchango wetu leo utasaidia katika katika kuboresha hali hiyo hapa Hospitali ya Rufaa ya Mwananyamala. Jitihada zetu hazitaishia hapa tutaendelea kufanyakazi karibu na jamii inayotuzunguka.”
Naye Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mwananyamala, Dkt. Sophinias Ngonyani aliipongeza Benki ya Exim kwa msaada huo, na kuongeza kuwa msaada umewafikia kwa wakati muafaka na kuziasa taasisi nyingine za kifedha na makampuni mengine nchini kuiga mfano huo.
“Kwa niaba ya Jamii ya Hospitali ya Mwananyamala, Ningependa kuelezea shukrani zangu za dhati kwa hatua nzuri mliyoichukua kuweza kutusaidia vitanda hivi ambavyo vitatumika kwa wakinamama ambao tunawathamini kwa kiasi kikubwa maishani mwetu. Mchango huu utasaidia Jamii ya Mwananyamala kwa kiaasi kikubwa  sana,” alisema Dkt. Ngonyani.
Dkt Ngonyani alisema kuwa kadri ya serikali inapojitahidi kuzipatia vifaa vituo vya afya, jitihada haziwezi kutoshereza mahitaji yote kwa ujumla katika hospitali hizi, ndiyo maana kuna haja ya wadau wengine, hususani makampuni kujitokeza na kuunga mkono jitihada hizo na kuweza kuleta mabadiliko chanya katika sekta ya afya nchini.
“Nawapongeza kwa utekelezaji wenu mzuri wa sera yenu ya kufanya shughuli za kijamii. Ombi langu kwa benki ni kwamba bado tunakumbana na changamoto nyingi kama hospitali ya rufaa, Nawaasa msichoke kutupatia michango yenu katika sekta hii nyeti iokoayo maisha ya watu wetu,” Dkt. Ngonyani aliongeza.

No comments: