Tuesday, May 06, 2014

MAMA SALMA KIKWETE KATIKA SHEREHE ZA KILELE CHA SIKU YA WAKUNGA DUNIANI

Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akipokewa na Rais wa Chama cha Wakunga Tanzania Ndugu Febby Mwanga mara alipowasili kwenye Uwanja wa Mnazi Mmoja kulikofanyika kilele cha maadhimisho ya siku ya wakunga duniani tarehe 5.5.2014.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akisalimiana na Ndugu Clavery Mpagama mara baada ya kuwasili Mnazi Mmoja kuhudhuria kilele cha siku ya wakunga duniani tarehe…
Mke wa Rais nMama Salma Kikwete akipokewa na Rais wa Chama cha Wakunga Tanzania Ndugu Febby Mwanga mara alipowasili kwenye Uwanja wa Mnazi Mmoja kulikofanyika kilele cha maadhimisho ya siku ya wakunga duniani tarehe 5.5.2014.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akisalimiana na Ndugu Clavery Mpagama mara baada ya kuwasili Mnazi Mmoja kuhudhuria kilele cha siku ya wakunga duniani tarehe 5.5.2014.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akipokea maandamano ya wakunga wakati wa kilele cha siku ya wakunga duniani yaliyofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja tarehe 5.5.2015.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akimsalimi mtoto Rahim mwenye umri wa miezi 2 akiwa na baba yake ndugu Amir Adam, 35, na mama yake Hamida (kushoto) walipompeleka kupata chanjo wakati wa sherehe za kilele cha siku ya wakunga duniani iliyoadhimishwa kitaifa katika viwanja vya Mnazi Mmoja tarehe 5.5.2014.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akitembelea mabanda mbalimbali yaliyokuwa yakitoa huduma ya afya ya mama na mtoto wakati wa kilele cha cha sherehe za siku ya wakunga duniani iliyoadhimishwa kitaifa mkoani Dar es Salaam tarehe 5.5.2014.
Wakunga mbalimbali na wananchi wakifuatilia kwa karibu hotuba mbalimbali zilizokuwa zikitolewa na viongozi wakati wa kilele cha siku ya wakunga duniani tarehe 5.5.2014.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwahutubia wakunga na wananchi waliohudhuria sherehe za kilele cha siku ya wakunga duniani iliyofanyika kitaifa hapa nchini kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja tarehe 5.5.2014.
Mke wa Rais akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Chama cha Wakunga Tanzania na baadhi ya wakunga waliohudhuria sharehe za kilele cha siku ya wakunga duniani tarehe 5.5.2014.
Picha na John Lukuwi.

No comments: